Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda, biashara na uwekezaji ni muhimu sana katika kuinua uchumi wa nchi yetu tunaomba Serikali kufufua viwanda vilivyokufa kwa kuzingatia gharama za kufufua viwanda hivyo. Kabla ya kuanza kazi ya kufufua viwanda hivyo, lazima kufanya cost analysis ili kujua gharama halisi ya viwanda hivyo, kama gharama ni kubwa ni heri kujenga viwanda vipya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa viwanda vipya, kabla ya kujenga viwanda vipya, Serikali lazima kuangalia maeneo ya kujenga viwanda hivyo. Vitu vya kuangala ni miundombinu kwa mfano, barabara, umeme, gesi, umeme na ardhi, Serikali ihakikishe inaboresha miundombinu ili kuwezesha usafiri na uzalishaji wa bidhaa unakuwa imara na unaboreshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya viwanda. Serikali lazima kutumia technology katika kuimarisha viwanda vyetu, vijana wetu lazima wasomee elimu ya kuendesha viwanda hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu soko. Serikali lazima ihakikishe inatafuta soko la bidhaa ambazo zitakuwa zinazalishwa katika viwanda. Tunajua Serikali haifanyi biashara lakini inaweza kuwezesha wafanyabiashara kupata soko la bidhaa zinazozalishwa katika viwanda vyetu. Viwanda ambavyo Serikali inaweza kuviboresha ni viwanda vya chai, korosho, pamba, ngozi, sukari na viwanda vya mbao ambavyo vipo Wilaya ya Mufindi katika Mkoa wa Iringa. Ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.