Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GEORGE M. LUBELEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri sana. Pili naunga mkono hoja hii kwa asilima mia moja, pamoja na kuunga mkono hoja hii naomba kuchangia yafuatayo:
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda; kwa kuwa wananchi wa Dodoma wanalima sana zabibu lakini hawana soko la kuuza na kiwanda cha kutengeneza au kukamua mvinyo wao ndiyo maana wananchi wanakata tamaa kulima zao la zabibu. Je? Serikali itawasaidiaje wananchi wa Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanda vidogo vidogo, kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma wanalima sana karanga, zao la alizeti na ufuta, lakini hawana viwanda vidogovidogo vya kukamua mafuta, Serikali isaidie wananchi hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.