Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu unajielekeza katika eneo la viwanda vidogovidogo kwani eneo hili likisimamiwa na kupewa kipaumbele litachochea na kukuza ajira, Wizara isimamie SIDO kuanzisha mitaa ya viwanda, mfano katika Jimbo la Mbagala Kata ya Chamazi, Charambe, Tuangoma, Kilungule na Kiburugwa zina maeneo ya kutosha kwa
ajili ya mpango huo, kutokana na idadi kubwa ya watu katika Jimbo langu naomba mpango huo utambuliwe na Wizara na kuanzishwa kwa haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Pili; mchango wangu unajielekeza katika uwezeshaji wa wajasiriamali wa kati na wa chini kabisa. Uwezeshaji huu utasaidia sana kuinua kipato, pia uwezeshaji wa zana kwa ajili ya kuanzisha viwanda vidogovidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tatu; Wizara ifanye uhakiki wa viwanda vilivyobinafsishwa kama vinafanya kazi kwa malengo yaliyokusudiwa kwani viwanda vingi vimebaki kuwa maghala na magofu mfano TANITA kiwanda kilichopo Mbagala kimegeuzwa ghala la kuhifadhia chupa chakavu. Serikali ikirejeshe kiwanda ili kiweze kuendelezwa kwa madhumuni yaliyo kusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Nne; kumekuwa na ongezeko kubwa la viwanda vidogo vidogo vilivyoanzishwa lakini vimekuwa hatarishi katika mitaa na maeneo ya makazi. Wizara ihakiki viwanda hivi ili visilete madhara katika jamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tano; Wizara iangalie uwezekano wa kuisaidia Halmashauri kujenga na kuboresha masoko yawe ya kisasa ili kutoa huduma bora na masoko yawe ya kisasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sita; Wizara ina hakika gani kupitia TBS kuhakikisha kuna mawakala wa ukaguzi wa bidhaa nje ya nchi mfano magari yaliyopo Uingereza, Japan, Dubai na kadhalika. Uhakiki wa mapato, ubora wa uhakiki huo, umakini na uaminifu wa mawakala hao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, natanguliza shukrani, nawasilisha.