Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo mambo machache sana ya kuchangia kama ifuatavyo:
Kwanza kabisa ni wavuvi wamekuwa wakichomewa nyavu zao ambazo ni haramu, nyavu hizo zimeendelea kwa kiasi kikubwa kuzalishwa na viwanda na kusambazwa na wanafanya biashara kila kona hapa nchini. Kwa kuwa, hali hii inaendelea kuwafanya wavuvi kuwa maskini, wengi wa wavuvi wanachukua mikopo benki na taasisi zingine za fedha kama PRIDE, FINCA, SACCOS na kadhalika. Kwa muda mrefu sasa Wabunge tumekuwa tukitaka Serikali ya Awamu ya Tano kukomesha uzalishaji na usambazaji wa nyavu hizo ili zisiwafikie wavuvi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua ni mkakati gani uliopo kuhakikisha kwamba, nyavu hizo haramu hazizalishwi na kusambazwa ikiwa ni pamoja na kudhibiti uingizaji wa nyavu hizo kutoka nje ya nchi? Naomba maelezo ya kina juu ya kuwepo kwa mkakati huo kama upo au la.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili; kwa kuwa nchi yetu ilianzisha mpango mahsusi wa uwekezaji wa EPZ wa kutenga maeneo ambapo baadhi ya maeneo Serikali ililazimika kuwaondoa wananchi. Je, mpaka sasa kwa nini eneo la EPZ Wilayani Bunda Mkoa wa Mara halijatekelezwa? Ni vema tukajua utaratibu wa uwekezaji katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuchangia hayo machache naunga mkono hoja!