Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote ni vema nikamshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye rehemu. Ninakupongeza pia Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kulisimamia Bunge hili Tukufu kwa umakini mkubwa. Pia nitoe shukrani zangu za dhati kwako kwa kunipatia fursa na mimi kuchangia kwa maandishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nichangie hapa “kufufua viwanda” na kufanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda. Ingekuwa busara kama kwanza tungefanya utafiti wa kina hadi tukaelewa chanzo cha kufa viwanda vyetu hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema kwanza tukaandaa miundombinu itakayowezesha Tanzania kuwa ni nchi ya viwanda kweli. Umeme bado ni tatizo, umekuwa siyo wa uhakika unakatika hovyo hovyo, maji pia ni tatizo ni vema tungeboresha miundombinu hii kwanza.
Mheshimwia Spika, ni vyema viwanda vyetu vikaanza na sekta hii ya kilimo kwani ni rahisi kupata malighafi. Tungetumia zana za kisasa sana pamoja na mbolea hata mbegu za kisasa ili kupata tija baadaye tukipeleka kwenye viwanda vyetu. Nyanya zipo kwa wingi, miwa ya kutosha na matunda mengine. Hata mpunga kama tutalima kisasa tutavuna vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenda kwenye viwanda vya general tyre. Mimi hapa napata mashaka kidogo, sidhani kama tutaweza kumudu soko vizuri.
Bahari yetu pia ina samaki wengi wa aina tofauti, samaki hawa wanavuliwa na wageni, ni vyema viwanda pia vikaangaliwa kushindika samaki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema Tanzania ya viwanda tunayotaka ikaangalia mapema kuimarisha bandari zetu zote ambazo zitaweza kutuunganisha vizuri, tuweze kuuza vizuri mali zetu zitokanazo viwandani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vema kabla ya kuanzisha viwanda tukaandaa mpango mkakati wa kuvilinda viwanda hivyo. Lakini pia ni vema kukawa na maelewano ya karibu sana baina ya Wizara ya Kilimo, Miundombinu, Biashara, Viwanda na Uwekazaji wakatengeneza “unit” ili wakafanyakazi kwa pamoja, kwa baadhi ya wakati ikawa ni rahisi sana njia za mawasiliano na kukamilisha kwa wepesi lile lililopangwa mashirikiano baina ya Wizara hizi yanahitajika ili tupate Tanzania ya viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.