Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda kuwapongeza Serikali na mpango wa Tanzania wa Viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa unapoongelea viwanda unahitaji infrastructure iliyokamilika ambazo ni umeme wa kutosha na barabara ya kupitika kwa urahisi ambazo tunaipongeza Serikali kwa kuliona hilo na mnalifanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia ya sasa hivi ni dunia ya processing, ni vizuri Serikali iweke utaratibu mzuri kwa wawekezaji wa ndani na wa nje, wakubwa na wadogo wa kuweza kuanzisha viwanda kwa urahisi ikiwezekana kuwe na one stop centre ya kumaliza taratibu zote za leseni na vibali mbalimbali. Vilevile Mheshimiwa Waziri lazima akae na taasisi zake na wawe na speed ya kuweka Mazingira mazuri kwa yeyote anayetaka kuweka kiwanda especially vya processing (processing Industry), napenda nimshauri Mheshimiwa Waziri akija kwenye majumuisho ni vizuri awaeleze na kuwaelimisha Wabunge kwamba viwanda vya zamani huwezi kuvifungua, Hata mashine zilizopo sidhani kama zina vipuri vyake maana yake ni teknolojia ya zamani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotakiwa kufanyika ni kuhakikisha viwanda vya zamani vinapatiwa Wawekezaji ambao wataleta mitambo ya kisasa na kuanza upya. Hatuwezi kujadili yote haya kuhusu Viwanda bila umeme wa uhakika. Ni vizuri Mheshimiwa Waziri awe na angalau taarifa za juu ni lini gesi yetu itakuwa tayari kuanza kutumika na kutoa umeme mwingi ambao utavutia wawekezaji kuja kuwekeza katika nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba pia Waziri aje atoe ufafanuzi kwa Waheshimiwa Wabunge kuwa Serikali haifanyi Biashara na Serikali haijengi Viwanda, kinachofanywa na Serikali ni kuweka mazingira mazuri kwa Wawekezaji wa aina yote kuweza kuwekeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa kuwa wabunge wengi wanasimama na kuomba Serikali iwajengee Viwanda nadhani wakieleweshwa nia ya Serikali wataweza kuwa katika mstari mmoja wa kauli yetu ya Tanzania ya Viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naunga mkono hoja.