Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nakushukuru kwa kunipatia fursa hii nami niweze kuchangia kwenye taarifa hizi mbili za Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nawapongeza Wenyeviti wetu wote kwa ripoti nzuri kabisa ambazo wamezi-table hapa. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti na nitaenda kujielekeza kwenye MSD, pale ambapo Kamati ya Bajeti tulitembelea tukagundua changamoto mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhahiri kabisa kwamba Taifa letu limekuwa likikumbwa na upungufu wa dawa kwenye hospitali na vituo mbalimbali vya kutolea huduma na suluhisho mojawapo ni haya ambayo nitaenda kuyasema, wala siyo yale ambayo Waziri alisema sijui kuondoa maduka ya dawa kwa mita 500. Unaweza kuondoa mpaka kilometa mbili, lakini bado kukawa na changamoto ya upungufu wa dawa, kama haya hayataweza kufanyiwa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mojawapo tumeshuhudia mlolongo wa utaratibu mzima wa ununuzi unachukua muda mrefu sana. Ni kwamba, mchakato wa zabuni tu unachukua miezi mitatu, baada ya pale kama unaagiza vitu kutoka nje itachukua miezi mitatu tena kufika baada ya kumaliza mchakato wa zabuni. Kama ni ndani ya nchi itachukua miezi miwili. Sasa ukijumlisha ni miezi mitano mpaka sita ili uweze kupata dawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ili tuweze kuepukana na huu mlolongo mrefu nilikuwa nashauri: moja, tuhakikishe Serikali inapeleka fedha kwa miezi minne walau mfululizo ili kukabiliana na huu mchakato mzima uweze kuji-absorb ndani kwa ndani kuhakikisha kwamba tunakuwa na consistency ya ku-supply dawa kwenye vituo vyetu vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ni kuhakikisha kwamba, walau tuweze kubadilisha sheria ili kwa dawa zile muhimu. Mchakato wa zabuni usichukue miezi mitatu, ungechukua hata mwezi mmoja kuhakikisha upatikanaji wa dawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine, Sheria yetu ya Manunuzi ya Umma pia inatambua kwamba mzabuni mwenye gharama nafuu ndiye atakayepewa tenda, yaani bila kuangalia uhalisia wa bei ya gharama husika kwenye soko. Hii inasababisha baadhi ya wazabuni kuweza hata kula njama, just a syndicate.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano, labda nataka ni- supply let say, X-Ray machines nyingi kwenye hospitali fulani na ninajua kabisa na John anafanya biashara hiyo na mwingine; unaweza ukawa na syndicate tu. Bei halisi kwenye soko unakuta labda ni shilingi milioni 50 kwa X-Ray moja, lakini sisi tuka-bid; nikaweka shilingi milioni 100, John akaweka shilingi milioni 120, mwingine akaweka shilingi milioni 130. Mimi wa shilingi milioni 100 nikachukuliwa wakati kiuhalisia bado tume-inflate bei, imekuwa kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, MSD wakalalamika sana kwamba wamefanya tafiti na wamegundua kabisa, unapokuwa unachukua ile tender, pamoja na kwamba inaonekana ni the lowest bidder, lakini kwenye uhalisia kwenye market unakuta wame-inflate price. Unaweza ukanunua kwa shilingi milioni 120 wakati kwenye market unakuta kitu kinauzwa shilingi milioni 60.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nashauri pia tuangalie hili, tubadilishe Sheria ya Manunuzi ya Umma walauo iweze ku-accommodate kipengele kiongezeke pale kwamba, sawa ni the lowest bidder, lakini tuangalie na uhalisia wa bei kwenye soko inakuwa ni kiasi gani? Vinginevyo tutakuwa tunapeleka gharama kwa walaji ambao ni Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, kuna huu mfumo wa manunuzi kwa njia ya mtandao (Tanzania Electronic Procurement System). Huu mfumo una upungufu ambapo unasababisha gharama kwa MSD. Huu mfumo unatambua lugha mbili tu; Kiswahili na Kingereza. Sasa ukiangalia watengenezaji wakubwa wa vifaa hivi, kwa mfano, MRI, CT-Scan, sijui X-Ray, na kadhalia, kwa mfano, ni Spain, Russia, German and the alike. Wachina ambao hii lugha ya Kiingereza siyo lugha yao ya mwanzo ukiingia kwenye mifumo yao ya system; kwa hiyo, inasababisha mwanya kwa huyu MSD asiweze kununua straight from the manufacturer, inabidi anunue from the supplier ambaye ana- act kama an agent.

Mheshimiwa Naibu Spika, huyu supplier anaweza akanunua kwa sababu yeye mfumo unakubaliana; anajua Kiingereza na Kiswahili; ananunua kwa producer au manufacturer kitu ambacho tungeweza kukinunua sisi straight; let say kwa shilingi bilioni mbili, yeye anakuja anatuuzia kwa shilingi bilioni 2.5 au shilingi bilioni 2.8.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tuangalie huu mfumo wetu tuurekebishe uweze ku-accommodate lugha zote ambazo tunajua kwamba tunanunua vifaa hivi vya hospitalini kuweza kupunguza gharama kinyume cha hapo tunatoa mwanya mkubwa na gharama kubwa kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine tulipotembelea pale tuliona kabisa kwamba kuna vifaa ambavyo vinatozwa kodi ya ongezeko la thamani na kodi ya maendeleo ya reli. Mathalani vifaa vya vifungashio vya madawa panadol, PVC unakuta vinatozwa kodi unakuta pia vinatozwa kodi ya ongezeko la thamani kwenye vipuli ambavyo ni vipuli vya muhimu sana au kwenye mashine ya vitendanishi ambavyo vinasaidia mathalani kwenye kutoa huduma ya uchujaji wa damu dialysis. Hivi ukitoza hivyo unapelekea bei inakuwa kubwa sana na Watanzania wengi hawawezi waka-afford bei hizi za huduma ya uchujaji wa damu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nilikuwa nashauri na ukitegemea Tanzania ili tuweze kuvutia wawekezaji nchi yetu ya Tanzania mojawapo ni kutoa hizi tax incentive. Kwa sababu vivutio vingine like umeme, ni shida bado kwetu hapa hatuna umeme ambao ni reliable muda wote ili wawekezaji waweze kuja achilia mbali hili taasisi ambayo ni ya Serikali. Maji pia ni shida miundombinu ya barabara na vingine vyote ni shida, sasa pale ambapo tunaona kuna umuhimu kwa maslahi ya Taifa kama hivi nilivyoeleza hapa hatuwezi kutoa exemption yaani tuondoe hii kodi ya ongezeko la thamani nah ii kodi ya maendeleo ya reli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mathalani kwa hawa wa Keko hawa MSD ambao wanasema ukiviweka hivyo inakuwa ni gharama sana sasa kwa kuanzia tuondoe hiyo tuone sasa tukishaondoa hii ambayo inaenda kupunguza gharama uzalishaji utaongezeka vipi kwa viwanda ambavyo ni vya Serikali. Tukishaona baada ya muda sasa tuweze kukaribisha na sekta binafsi kupitia PPP ili waweze kuingia na wenyewe kwa kufanya hivyo ina maana tutakuwa na viwanda vingi ambavyo vinazalisha madawa haya na tutaenda kupunguza ukosefu wa madawa kwenye vituo vya afya, kwenye hospitali na kuweza kuokoa maisha ya watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine kwa haraka haraka Mheshimiwa Naibu Spika na wewe ulikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje by then Ulinzi na Usalama, na tulikuwa na kikao Kamati ya Uongozi moja ya issue ambayo ilijitokeza zaidi ilikuwa ni fidia ambazo wanatakiwa walipwe watanzania wanaopisha maeneo kwa ajili ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na katika Kamati ya Uongozi siku zile tuliazimia na Serikali ikasema kabisa inaenda kufanya hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka sasa hivi yale maeneo yaliyoainishwa ya Viruti, sijui Kikombo, Nyabange na maeneo mengine ambayo pia yaliahidiwa kwamba yangeweza kutekelezwa by then mpaka kufikia muda huu ikiwepo Tarime ambayo kila siku nasimama naongea hapa tunaomba Serikali muweze kufanya fidia ili hawa wananchi Watanzania hawa waweze kuondoka kwenye hayo maeneo waende kwingine wakafanye shughuli za maendeleo wamekuwa wamekaa kama watumwa kwa muda mrefu sana mnafanya tathmini muda unapita muda unapita unarudi tena kufanya tathmini. Si sawa kabisa tunaomba kabisa kama vile ambavyo kamati imeainisha na kikao kilikaa Serikali iweze kupeleka fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa ni hili pendekezo la kuhakikisha kwamba tunaongeza fedha kwa ajili ya TARURA na hii imekuwa ni vilio sana hatuna muunganiko kwenye maeneo yetu huko si vijijini si mjini hata hapa Dodoma ukipita kwenye barabara hizi ambazo ziko under TARURA ni disaster. Sasa Serikali iweze kulichukua hii ihakikishe imeongeza hizo walau bilioni 111.3 kwa Kunzia kwa kuweka installment mwezi huu na mwezi ule ili uhakikishe kwamba tunaweza kurekebisha hizi barabara.

Lakini in future kama ambavyo Waziri wa TAMISEMI hapa juzi aliongea tuhakikishe kwamba haitokezi hii kitu muweze for cast muone kabisa kwamba huwa mvua ikitokea barabara zinaharibika kwa hiyo mtengeneze kwa kiwango ambacho kinakubalika.