Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa kunipa dakika tano niseme niliyokuwa nimepanga kusema. La kwanza, namuunga mkono Mwalimu Bilago kwamba hili suala la watoto wa kike wanaopata mimba wanaachwa bila kushughulikiwa amelichokoza leo kwa Waziri anayehusika na usawa wa jinsia, namwomba na nawaomba Waheshimiwa Wabunge tulirudishe wakati Wizara ya Elimu itakapokuja kuleta bajeti yake hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nawaunga mkono Waheshimiwa Wabunge wote waliosema kwamba vifaa vinavyowasaidia akina mama na wasichana kujihifadhi vipunguziwe kodi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi kwa upande wa Urambo. Kama walivyosema vifo vya akinamama tunaweza kuvipunguza pale ambapo tu kutakuwa na mkakati maalum, nami naamini Waheshimiwa Mawaziri waliochaguliwa wana uwezo, mwakani watakuja na mikakati mizuri zaidi, hongereni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue mfano kwa upande wa watumishi, tazama Urambo ilivyo, tuna zahanati 20, ni zahanati tano tu ambazo zina Matabibu. Sasa unategemea nini anapopelekwa mwanamke mwenye mimba ambaye ameshindwa kujifungua kwenye zahanati 15 ambazo hazina Matabibu? Pia kama walivyosema wenzangu, kuna mradi wa ADB, umetuacha sisi Urambo na Zahanati ya Wilaya; nusu imejengwa, pia theatre kwenye upande wa Kituo cha Afya, Usoke imeachwa nusu kwa upande wa Usoke na Isongwa; kliniki zilizokuwa zinajengwa, zimeachwa nusu halafu Serikali inatuambia sisi wenyewe tumalize, haiwezekani! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sisi wote Wabunge ambao tumeguswa na huu mradi wa ADB tufanye mpango wa kuona Serikali itajibu nini kuhusu kutuachia jukumu la kumaliza majengo ambayo yapo nusu. Pia chukua kwa mfano, wenzangu wamezungumzia juu ya OC zilivyopunguzwa, mwaka 2015 Urambo ilipewa shilingi milioni 185, mwaka huu imepewa OC milioni 60. Jamani itafanya kitu gani? Kulisha wagonjwa na kila kitu! Kwa hiyo, tunaiomba Serikali iangalie jinsi ambavyo inakata mambo mengine ambayo yataathiri sana afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia On call Allowance kwa mfano Urambo tangu Januari mpaka leo hawajapata On call Allowance, mnategemea wafanyakazi watafanya kazi kwa moyo kweli! Kwa hiyo, tunaomba On call Allowance zipelekwe ili wenzetu waweze kufanya kazi kwa moyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wafanyakazi wapya wanaopelekwa kwenye wilaya hizi hawapelekewi fedha za kujikimu kabla hawajafika. Kwa hiyo, hilo nalo tunaomba litendeke. Pia Wilaya ya Urambo haina gari la chanjo. Tunaomba gari la chanjo, Mheshimiwa Waziri atakapojibu atuambie lini angalau watu wa Urambo tutapata gari la chanjo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naunga mkono wenzangu waliosema mfumo wa watumishi katika Wizara ya Afya uangaliwe upya. Kwa mfano, sisi tumepata kibali cha kuajiri, lakini tuliomba kibali wakasema mtaajiri, lakini eti tunaambiwa tusubiri mpaka Wizara itangaze. Itatangaza lini? Tunaomba Serikali ituambie ni lini Serikali itatangaza ajira? Kwa sababu kama nilivyowaambia ni kwamba, tuna Matabibu watano tu katika zahanati 20, lakini wametuacha tusubiri mpaka Wizara itakapotangaza. Kwa hiyo, naunga mkono wenzangu waliosema kwamba mfumo wa kuhudumia watumishi ndani ya Wizara au Sekta hii ya Afya uangaliwe upya, inawezekana pengine tukahitaji mfumo mzima ubadilishwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu sasa kutokana na maingiliano ya majukumu inakuwa ni vigumu sana kuajiri kwa wakati, mambo ambayo yangeweza kufanyika ndani ya TAMISEMI, unaambiwa yasubiri huko juu. Kwa hiyo, nami naunga mkono kwamba mfumo mzima uangaliwe wa jinsi ya kuhudumia watumishi ndani ya Halmashauri zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naangalia hivi vifo vya akinamama, ndugu zangu, ni vita! Kila siku wanawake 42 wanakufa! Kungekuwa labda na uwezekano wa hawa akinamama 42 kila siku wakazikwa pamoja, nadhani lingekuwa shamba la ajabu kabisa kwa sababu kama kila siku ni 42 kwa mwezi ni elfu moja mia tano na ngapi huko! Kwa hiyo, ingekuwa hata pengine tunakwenda kuzuru sisi, kuwasalimu wenzetu ambao wamefariki wakifanya wajibu wao waliopewa na Mwenyezi Mungu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri wa Afya aje na mkakati mzuri zaidiā€¦