Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru kwa kupata muda wa kuchangia kidogo katika Wizara hii ya Afya. Kwanza kabisa, kwa haraka nampongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri sana wanayoifanya, tunaahidi tupo nyuma yeo, tunawaunga mkono kwa kazi nzuri wanayoifanya. Tunajua wana jukumu zito mbele yenu, lakini Mungu atawasaidia, watafanya kazi nzuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Waziri, Wilaya yetu ya Uyui tulileta maombi ya zahanati zetu mbili kuona uwezekano wa kupandishiwa hadhi kuwa vituo vya afya, nashukuru sasa mchakato umekamilika, zahanati ya Ilolangulu na Malongwe zinapandishwa hadhi kuwa vituo vya afya. Tunaomba mchakato wa kupata barua na kuingizwa kwenye bajeti ufanyike ili vianze kufanya kazi. Nashukuru sana kwa hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie mambo mawili au matatu kuhusu uhaba wa dawa kwenye zahanati zetu. Uhaba wa dawa ni mkubwa sana, tunaomba juhudi zinazofanyika zizidi kufanyika sawasawa ili zahanati zetu zipate dawa za kutosha ili wananchi wetu wanapokwenda kupata matibabu waweze kutibiwa na kupata dawa katika zahanati zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua juhudi kubwa inafanyika sasa lakini pamoja na dawa muda mwingine kufika kwenye maeneo yetu, udhibiti wake unakuwa ni mdogo, wajanja wanazitumia vibaya tofauti na matarajio. Tunaomba pia udhibiti wa dawa hizi zinapokuja kule ufanyike sawasawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nami kama walivyoomba wenzangu, kwanza naipongeze MSD, tunatarajia kutenga pesa kulipa deni lao kubwa ili kuwawezesha kufanya kazi zao vizuri sana. Naomba tuweke pesa zaidi kulipa deni lote ili kuwafanya waweze kutoa huduma ya dawa vizuri zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia maduka ya MSD ambayo yanafunguliwa katika Hospitali za Mikoa, ni wazo zuri na tunalipongeza, lakini sasa Wizara ifikirie kuona namna MSD itakavyofungua maduka haya kwenye Wilaya zetu. Kwenye Hospitali za Wilaya ambapo ndiko kuna wagonjwa wengi na wananchi wengi wanatibiwa katika hospitali zetu za Wilaya, yakifunguliwa maduka huko, itasaidia huduma hii kuwafikia wananchi wetu wengi tofauti na maduka haya kuishia kwenye hospitali za mikoa peke yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie huduma za wazee. Sera ya Huduma kwa Wazee Kutibiwa Bure, inatakiwa itengenezewe utaratibu mzuri zaidi. Hii sera ipo, lakini practically haifanyiki hivyo, wazee wetu wanateseka, wakienda hospitali zaidi ya kuandikiwa panadol hakuna dawa wanazopata.
Wakati mwingine kwa sababu hawatoi pesa, hata huduma wanazopata zinakuwa za kusuasua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara isimamie hili, kwa sababu kama Mheshimiwa Waziri alipokuwa anazungumza katika hotuba yake anasema mzee alikuwa kama sisi na sisi tutakuwa kama yeye hapo baadaye, kuna haja ya kuangalia wazee wetu kwa macho mawili zaidi ili wapate huduma ambayo inastahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, huduma za mama na mtoto, kwa asilimia kubwa wanaokwenda kupata matibabu katika zahanati zetu ni wazee, akinamama na watoto. Sera inasema watapata matibabu ya bure, lakini naomba tena hapa, Mheshimiwa Waziri atakapokuja atueleze ni mkakati gani anataka kuuweka sasa ili kusaidia huduma ya mama na mtoto katika zahanati zetu huko chini, ikiwemo pia na upatikanaji wa dawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda, nizungumze la mwisho. Tumepata hamasa ya kuwaambia wananchi wetu wajenge zahanati katika maeneo yetu. Tumejenga zahanati za kutosha lakini hatuna wauguzi katika zahanati nyingi. Kwa sasa vijana wetu wengi wanahitimu Udaktari na Shahada mbalimbali katika fani ya Udaktari na utabibu, lakini hawaajiriwi na Serikali yetu ili kufanya kaziā€¦