Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kuwashukuru baba zangu, mama zangu wa Jimbo la Bunda Mjini kwa unyenyekevu mkubwa, bila kujali umri wangu, bila kujali jinsia yangu, mkasema ng‟wana Bulaya ndiye chaguo sahihi la Jimbo la Bunda Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushindi wangu umetoa fundisho kwa wale wote wenye kiburi cha kukaa madarakani muda mrefu. Pia ushindi wangu umetoa fundisho, wananchi wataangalia product bora inayopelekwa na chama husika na si ukubwa wa chama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba nitoe pongezi kwa Msemaji wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Wale ma-senior kama mimi asilimia 30 tuliorudi, mnajua kwamba isssue si Mipango, issue ni utekelezaji wa Mipango. Issue si Serikali ya awamu hii, ni utekelezaji wa Serikali husika. Issue si Ilani ya 2015, ni utekelezaji wa Ilani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia tena mapinduzi ya viwanda. This time don’t talk too much, fanyeni kazi. Rais wa Awamu ya Nne alipokuwa akizindua Bunge, alisema mapinduzi ya viwanda, kwenye Ilani ya mwaka 2010 ukurasa 171, imezungumzia mapinduzi ya viwanda. Hatuhitaji tena mzungumzie, tunahitaji mtende. Tunataka mtende! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sio kwetu sisi tu, Taifa hili linatuangalia, tutembee kwenye maneno yetu. Wenzetu wanachukua Mipango yetu wanaenda ku-implement kwenye nchi zao. Please, wapeni Watanzania wanachokitarajia. Tuache kusema, tutende. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na Wabunge wote waliozungumzia reli ya kati na naungana na hoja ya kuhakikisha tuna viwanda, tuvifufue vya zamani, tuwe navyo. Ni jambo la msingi sana, lakini leo hii tunazungumzia mapinduzi ya viwanda. Tumemaliza ujenzi wa VETA kila Wilaya? Mambo haya yanakwenda sambamba. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ma-graduate wenye masters, wenye degree wale ni ma-superviser. Tunahitaji kuandaa product nyingine ya certificate, ya diploma tuipeleke kwenye viwanda. Tunatakiwa tuwe na VETA, VETA na mapinduzi ya viwanda yanaenda sambamba. China ilifanikiwa kwa mtindo huo. Please tuwe na VETA, tuwe na viwanda, tunatoa watu huku kwenye VETA tunaingiza viwandani tunatatua tatizo la ajira kwa vijana. Tupange kwa makini, tutekeleze kwa makini kwa maslahi ya vijana wa sasa na wajao, please mkaangalie tena. Tusiseme tu VETA kwenye kila Wilaya ziko wapi tumezungumza miaka mitano iliyopita, this time mara ya mwisho tuongelee mapinduzi ya viwanda Watanzania waone viwanda si maneno, do not talk too much, tendeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtakapoamua kwenda kuwekeza kwenye viwanda, kuna mmoja alisema angalieni na jiografia, sisi kwetu kule Kanda ya Ziwa hatuhitaji katani kule ni pamba, ng‟ombe na uvuvi. Hiyo niliyosema ya VETA mwenye degree ataenda kusimamia samaki wanasindikwa vizuri yeye hataenda kusindika. Mwenye degree, mwenye masters hataenda kutengeneza viatu atasimamia viatu vimetengenezwa vizuri, ni ushauri chukueni ufanyieni kazi. Hamtaimba tena 2020 hapa, fanyeni kazi siyo maneno, it is not about slogan ni utendaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mlikuja hapa na Maisha bora kwa Kila Mtanzania yako wapi? Leo hapa kazi iko wapi? Siyo maneno ni vitendo. Siyo tu wingi kwa kuandika kwenye Ilani mmeziandika sana tendeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tumezungumzia kuhusiana na Shirika letu la Ndege jamani kuwa na Shirika la Ndege ni ufahari tukiwa kwenye nchi za wenzetu. Tunapishana tu na ndege za Kenya, Rwanda, sisi tunasema tu tutafufua, tutafufua lini? Nchi ndogo kama Malawi wana ndege. Baba wa Taifa aliacha ndege tunahitaji ndege. Mnaenda Dubai mnapishana na ndege za Kenya, Rwanda na kadhalika tunahitaji ndege. Kuwa na ndege jamani unachangia pia kwenye sekta ya utalii, watu mnaosafiri mnajua. Ukishuka pale Kenya wazungu wote wanaishia Kenya halafu wanakuja Kilimanjaro, tungekuwa na ndege wangeshukia Dar es Salaam fedha zile wanazoziacha Kenya wangekuja kuacha kwenye nchi yetu lakini ndege moja, sijui mtumba kila siku tunazungumzia ndege, ndege ziko wapi? Kwa nia njema tutende ili tulitendee haki Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunapozungumzia sekta ya utalii watu wanajua utalii ni tembo tu, siyo tembo, wenzetu kule wametengeneza visiwa, sisi mashallah Mungu ametupa hatuhitaji kuvitengeneza, tunavitumia kwa aina gani vile visiwa? Tunaboresha maeneo yetu mengine ya utalii, tuna Mbuga pale ya Saa Nane, ukienda kule unaona Mwanza nzima jinsi ilivyo nzuri lakini cha kushangaa hata hoteli kule hatuna. Tungetengeneza huu Ukanda wa Kaskazini na Kanda ya Ziwa ungekuwa sekta ya utalii. Mtu anatoka Ngorongoro, anaenda Serengeti, anaenda Saa Nane anaenda kwenye visiwa vyetu ambavyo Mungu ametujalia. Wenzetu nchi nyingine wanatengeneza visiwa na maeneo ya utalii lakini sisi tunayo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ashakum si matusi wengine wanasema visiwa vyetu wanaenda kujificha wake za watu na wanaume za watu. Visiwa vyetu tunatakiwa tuvitumie kwenye utalii ndugu zangu. Tunayaongea haya kwa uchungu mkubwa, Mungu ametupa mali hatuzitumii. Haya ni mambo ya msingi tumeyasema na Mwenyekiti wewe ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maliasili na Utalii. Watu wanakuja wanayalalamikia haya, mambo kama hayo lazima tuyaweke katika mipango yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie deni la Taifa, nakubaliana kabisa hakuna nchi isiyokopa. Kukopa ni jambo lingine, kwenda kuwekeza katika kile ambacho wamekikopea pia ni jambo lingine. Leo hii tunadaiwa US Dollar milioni 19. Nimesema kukopa siyo shida, je, tunazitumiaje hizo fedha tunazokopa? Tunakopa tunaenda kuwekeza kwenye eneo gani? Fedha zetu za ndani tunaweza kuwekeza katika maeneo ya huduma za kijamii hizi fedha tunazokopa twende ku-invest katika maeneo ambayo yatazalisha na tutaweza kulipa deni kwa mujibu wa mikataba tuliyoingia na kuondokana na mlundikano wa riba kama ambavyo upo humu kwenye ripoti. Hilo ni jambo la msingi sana. Tatizo hata katika hii Mifuko yetu ya Hifadhi ya humu ndani ambayo tunaikopa na hatuilipi, tunaenda kuwekeza sehemu ambazo hatuzalishi. Hilo ni jambo la msingi ukikopa nenda kawekeze eneo ambalo litakuwezesha kulipa deni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba mtende, msiendelee kuongea, ahsante. (Makofi)