Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kukushukuru sana. Kwanza naunga mkono asilimia mia moja hoja hii ya Waziri wa Ulinzi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Jeshi la Wananchi wa Tanzania lina history kubwa sana duniani siyo Tanzania tu. Jeshi hili limefanya kazi kukomboa nchi nyingi sana chini ya Jangwa la Sahara. Jeshi hili la Tanzania limefanya kazi kwa uadilifu na kwa ujasiri mkubwa sana kukomboa na kufanya kazi Afrika. Mimi nampongeza sana Mkuu wa Majeshi na Makamanda wake wote kwa namna walivyotuweka na namna walivyoweka nchi hii kuipa heshima. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Jeshi hili ni jeshi kubwa sana mpaka Umoja wa Mataifa wanalitumia kwenda kulinda amani nchi zingine. Jeshi hili ni imara na linafanya kazi kwa kiwango kikubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba kumkumbusha Mheshimwa Waziri, mimi nilikuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje kwa miaka kumi toka mwaka 2005 mpaka 2010. Tumejenga hoja na tumekubaliwa na tukaambiwa na tuliishauri Serikali pensheni za vyombo vya ulinzi zitolewe kwenye utumishi wa kawaida, Serikali walikuwa tayari wameshaandaa Muswada kuja Bungeni, lakini walikuwa wanasubiri kidogo wenzao wa upande wa pili na wao waweke inputs zao. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ninamuomba Mheshimiwa Waziri kipindi sasa kimefika, siyo jambo zuri kuona vikosi hivi au wanajeshi wetu, maafisa na wapiganaji kutokupata pensheni nzuri sababu tu ya mfumo wa utumishi uraiani. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri nitakuomba utueleze leo mmefikia wapi kuhusu kulifanya sasa Jeshi la Ulinzi na vyombo vya ulinzi kwa ujumla, viweze kupewa pensheni maalum kwa heshima na kazi kubwa wanayoifanya kwa Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, najua Serikali ina nia njema na tunaamini ina ina nia njema, tunaomba sasa nia njema ile iwekwe ili iweze kuwasaidia wanajeshi hawa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nchi nyingine kwa mfano Asia, majeshi yanapewa miradi maalum yaweze kujiendesha na kusaidia mapato wanayopata kwenye miradi ile waweze kusaidia kujiendesha kwa namna ambayo wanaona inawafaa. Kuna nchi ya Asia, majeshi yamekabidhiwa kwa kwetu hapa tunaita National Housing, sijui kwa kwao wanaitaje, karibuni nyumba nyingi za mjini nchi zingine zimeachiwa jeshi kuziendesha ili na wao waweze kunufaika.
Mheshimiwa Spika, najua kuna miradi siku za nyuma walipewa Jeshi, najua kulitokea matatizo lakini siyo sababu ya kuwanyima kuwapa fursa hiyo wao kuendesha miradi ili waweze kupata heshima na waweze kujipatia kipato cha kuendesha mambo yao.
Mheshimiwa Spika, nchi zote duniani Jeshi linashirikishwa kwenye masuala ya Contagious Disease Centre (CDC) lazima jeshi liwepo. Sasa sidhani kama kwetu wanashirikishwa. Jeshi wanatakiwa washirikishwe kwenye tafiti mbalimbali za kilimo, afya na za magonjwa; ndiyo wao wenye utaalamu wa kuweza kuchambua na kuisaidia Serikali kufanya tafiti bora, Jeshi letu lina uwezo mkubwa sana wa kufanya mambo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tuliomba kwenye Kamati yetu ya Ulinzi siku za nyuma kuwa Jeshi sasa lipewe jukumu la kufanya doria na kulinda ridge ambazo zipo baharini zinazotafuta tafiti za gesi. Ma-ridge hayo ya ajiri makampuni kutoka nje, wanatumia silaha nyingi sana katika maji yetu na sidhani na kama ipo control, fine, lakini tunazungumzia pato ambazo Jeshi letu lingeweza kupata kwa kufanya doria kwenye ridge hizi ambazo zipo kwenye maji ya Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Jeshi lina uwezo wa kupata mapato makubwa sana badala ya pesa hizi kutumiwa na makampuni ya nje kama Black Water na makampuni mengine ambayo yanakuja kulinda na yanalipwa pesa nyingi sana. Insurance hii inalipwa na Serikali ya Tanzania kwenye gharama za kutafuta gesi hii. Ni bora sasa na naamini kwa vifaa ambavyo tunavyo, Jeshi sasa lina qualify kwa asilimia mia moja kulinda bahari zetu, kulinda na mitambo hii ya ridge ya tafiti za gesi ili kuongeza usalama lakini vilevile kupata mapato ili na wao waweze kujiendesha. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nilikuomba muda mfupi tu kwa sababu mara nyingi sichangii maneno mengi huwa nachangia point tu ambazo ni muhimu. Nitamuomba Mheshimiwa Waziri atupatie majibu haya.
Mheshimiwa Spika, lakini niendelee kusema Bunge hili tuendelee ku-support Jeshi, Bunge hili tuendelee kusaidia maslahi ya wanajeshi. Bunge hili lisaidie Jeshi letu liendelee kung‟ara Afrika na Mataifa ya nje. Lidumu Jeshi letu, idumu Tanzania.
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.