Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

Hon. Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2022

MHE. VITA R. KAWAWA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuhitimisha hoja niliyowasilisha asubuhi hii ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ya Kamati ya NUU - Nje, Ulinzi na Usalama imechangiwa na wachangiaji Tisa, nikianza na Mchangiaji wa kwanza alikuwa Mheshimiwa Mbogo ambaye alizungumzia diplomasia ya uchumi, alieleza Mikoa ya pembezoni mipakani ipewe elimu ya diplomasia ya uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati tulishatoa mapendekezo kwamba Bunge liazimie Serikali iandae mpango mkakati wa utekelezaji wa kidiplomasia ya uchumi nchini ikiwemo kuwapa elimu ngazi za Mikoa na Wilaya. Tunashukuru Wizara hapa imejibu na kuomba iruhusiwe ipate kuanza na mkakati mmoja, nasi kwa niaba ya Kamati tunakubali hilo. Pili, kupatiwa fedha Wizara ya Mambo ya Nje kukarabati Balozi zetu na kujenga, Kamati tulishatoa mapendekezo kushirikisha sekta binafsi, na sekta za umma katika ujenzi wa majengo ya Balozi na vitega uchumi kutarahisisha upatikanaji wa fedha na ujenzi wake kukamilika kwa haraka na hivyo kuwa na majengo ambayo yanastahili kwa hadhi ya nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wa pili, alikuwa Mheshimiwa Felister Njau, yeye amesisitiza upatiakanaji wa fedha zilizotengwa na kuidhinishwa na Bunge, kwamba mtiririko wake hauridhishi kwa Wizara zetu tunazo zisimamia, Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kwa hili mimi sina la kusema zaidi, ninaamini Serikali imekusikia na ninaamini italifanyia kazi. Kwa nyongeza tu Bunge linapotoa maazimio kuhusu mambo mahsusi linafanya kazi hiyo ili kuhakikisha kwamba tija iliyokusudiwa inafikiwa kwa ustawi wa wananchi. Hivyo ulinzi na usalama wa raia ni ustawi wa wananchi wake. Tukiwa na amani ndivyo hata tunaweza kufanya kazi nyingine. Hata hivyo, tuko hapa Bungeni kwa sababu ya ulinzi na usalama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ni vyema sana Bunge linapotenga na kuidhinisha fedha kwa ajili ya vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, tunaiomba Serikali ivipe kipaumbele vyombo vya ulinzi na usalama ili waweze kufanya kazi yake inavyotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Faharia pia alizungumzia PAROLE; Kamati ya NUU ilikwishatoa maelekezo kwa Wizara ya Mamabo ya Ndani ya Nchi kufanya tathmini ili kubaini changamoto ya utekelezaji wa Sheria ya PAROLE ili kuchukua hatua stahiki kuziboresha. Hata hivyo alizungumzia kuhusu Sera ya Mambo ya Nje; ni matumaini yetu Kamati na Bunge, Serikali itakamilisha maboresho ya Sera ya Mambo ya Nje mapema kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Condester Sichalwe, naye alizungumzia kuhusu COMESA. Serikali imesikia na imetoa ufafanuzi hapa; ila ushauri wetu sisi kama Kamati, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ije kutupa elimu, kutueleza kwa kina ili tuwe na uelewa wa pamoja kuhusiana na hii COMESA. Kwa sababu Mheshimiwa Waziri amepata muda mchache akalielezea kwa uchache; lakini kama akipata nafasi tunaomba uweze kuja na timu yako kulielezea Bunge kuhusiana na huu mtangamano na kujitoa kwetu COMESA na nini maana yake. Hata hivyo, tunafahamu kuna hii Tripartite, kuna EAC na SADC. Faida tunazozipata umezielezea hapa kwa ufupi. Hata hivyo, tungependa pia ungekuja kulielezea Bunge zima kama semina ili liweze kuelewa kwa makini kuhusiana na hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, Neema Lugangira, yeye alizungumzia ni lini Serikali itakamilisha mchakato wa diaspora kupata hadhi maalumu? Nadhani Waziri amelijibu vizuri suala hili, lakini sisi kama Kamati tunasisitiza Serikali ikamilishe mchakato huo ili hii kazi iweze kuendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Chumi naye alieleza kuhusu vijana waliopelekwa Israel kusomea kilimo cha kisasa, kwamba wanaporudi waunganishwe na vijana wa JKT na block farming zinazoanzishwa na vijana wengine. Mheshimiwa Chumi hili naamini Serikali imekusikia na naamini watalifanyia kazi. Serikali ina wajibu pia wa kuisaidia NIDA. Hoja yake ya pili, kuhakikisha inakamalisha utoaji wa vitambulish. Ni kweli, Kamati inaishauri Serikali kuendelea kuiwezesha NIDA kwa wakati ili kukamilisha zoezi hili; na tumesisistiza sana jambo hili liweze kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo Mheshimiwa Getere pia aliongezea kwenye hili, alisema tuambiwe ni lini kazi ya kutoa vitambulisho inakamilika au inaisha lini kazi hii? Ushauri wa Kamati, Serikali iendelee kuipatia fedha kwa wakati NIDA kama zilivotengwa na kuidhinishwa na Bunge ili kuharakisha utambuzi, usajili na kuchapisha vitambulisho na kuvisambaza kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Londo naye alitoa ushauri kuhusu diplomasia ya uchumi. Kamati imepokea ushauri wake na tunaamini Serikali pia imemsikia ushauri wake, na kama haikumsikia vizuri, basi tunaomba iitishe Hansard ili iweze kumsikia na kuona jinsi gani ya kutekeleza ushauri wa Mheshimiwa Londo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile Mheshimiwa Ally Kassinge naye alizungumzia mtiririko wa upatikanaji wa fedha katika vyombo vyetu vya ulinzi na usalama. Mimi ninaamini Serikali na Wizara ya Fedha, hususani Wizara ya Fedha imekusikia vizuri sana. Hata hivyo Kamati inapendekeza maazimio na haya yote ambayo yamo tunaomba Bunge liridhie ili yawe maazimio ya Bunge na Serikali iyafanyie kazi. Maazimio yetu yote tuliyoomba tunaomba Bunge liweze kuridhia ili yafanye kazi

Mheshimiwa Mwenyekiti, wachangiaji wengine walikuwa Waheshimiwa Mawaziri, Mheshimiwa Bashe Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Engineer Masauni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Stegomena Tax Waziri wa Mambo ya Nje, Mheshimiwa Innocent Bashungwa Waziri wa Ulinzi na Mheshimiwa Dkt. Mwigulu, Waziri wa Fedha. Tunawashukuru sana wote mliochangia mchango huu na ninaamini Serikali imewasikia vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo baada ya kutoa ufafanuzi wangu naomba sasa kutoa hoja kwamba, Bunge lako Tukufu likubali taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Pamoja na maoni na mapendekezo yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.