Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kupata fursa hii ili niweze kutoa maoni yangu. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Joseph Mbilinyi Msemaji wa Kambi ya Upinzani, juu ya habari lakini niwapongeze sana pia wale ambao walishirikiana nao kuandaa mambo mazito namna hiyo, nafikiri Mheshimiwa Nape atakuwa amesikiliza hiyo misumari na ataifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nachangia kwenye Wizara ya mtu ambaye ninamfahamu vizuri na imetangazwa hapa kwamba ni shemeji yangu kwa sababu mke wake anatwa Rhobi na Mheshimiwa Nape hatukukutana barabarani, ni kweli kwamba ni shemeji yangu sasa nitaomba Dada yangu Rhobi ninapochangia kwenye hotuba ya mume wake Mheshimiwa Waziri kwa sababu tupo kazini na tumeshachukua mahari, biashara ya ushemeji itakaa pembeni kidogo, hapa kazi tu, kwa hiyo tunaenda na kauli mbiu ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilisema nitakuwa mkweli sana, nimejaribu kutafakari kitu gani nichangie kwenye hotuba hii nikapanga haya yafuatayo niyaseme.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza Mheshimiwa Nape akiwa Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi aliwaita wenzake ni mizigo akiwepo Mheshimiwa Profesa Maghembe, Mawaziri wenzake wale aliowaita, kwa hiyo nilipoona amepewa Wizara ya Habari nikatarajia kwamba ataruhusu mijadala ya wazi ili tumuone kwamba yeye hatakuwa mzigo lakini anaweza kwa lumbesa ili tumjadili na wananchi wamuone. (Makofi)
Sasa hilo amelizuia kwa hiyo tunashindwa kumpima yeye na wenzake nani mzigo zaidi, nani lumbesa hilo na lenyewe kidogo linaleta shida. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili Mheshimiwa Nape atakumbuka kwamba wakati nilipokuwa nimeminywa sana kutoa maoni yangu kama kijana msomi kutoka Chuo cha Dar es Salaam, nikapingana na viongozi wa CCM nilipofikiria kuhama CCM Mheshimiwa Nape nilimshirikisha akiwa na Mheshimiwa Kubenea, tulienda kule Kitunda nikamwambia hawa watu ndugu zako, hawa viongozi wa CCM hawa wamenikwaza kwa sababu wamezuia uhuru wa kuzungumza, kutumia akili zangu kitaaluma kama mwalimu tena mwalimu wa Hesabu na Kemia. Kwa hiyo nikamwambia mimi nahama akaniambia safari njema.
Kwa hiyo, anajua wakati nahama Mheshimiwa Nape alikuwa anafahamu. Kwa sababu msimamo ule ule ambao tulitofautiana kule na wenzake yeye ameurejea tena, kwamba hatuwezi kuwa na uhuru wa kutoa maoni hapa na yeye ndiyo msemaji. Nimepitia taarifa yake hapa ameeleza vizuri kwamba yeye ndiyo anasimamia vizuri Wizara hii na kusema akifanya kazi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi mojawapo ambayo Mheshimiwa Waziri anasimamia moja, alikiri hapa kwamba hiki kinachoendelea hapa Bungeni cha waandishi wa habari wa TBC kufanya kazi hapa Bungeni alikiri kwamba ni kweli wametoka TBC maana yake kwenye Bunge hili hao wanaozuia taarifa na ku-censor tunachozungumza Mheshimiwa Nape ana mkono wake, kwa hiyo hawezi kukataa na alikiri kwamba hawa watu wapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimefuatilia mara tatu usiku, mara ya kwanza niliamka saa 7.42 usiku na juzi ile nikakuta ndiyo TBC inaonyesha taarifa ambayo imerekodiwa. Siku iliyofuata niliamka saa 8.15 usiku nikakuta tena wanaonesha, juzi nimeamka saa 9.40 usiku maana yake saa kumi kasoro dakika ishirini nikakuta ndiyo wanaonesha taarifa, nikaenda mpaka saa kumi ilikuwa inaendelea. Usiku wa kuamkia leo niliamka saa 7. 17 usiku nikakuta wanaonesha ile taarifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, maana yake ni nini! Mheshimiwa Nape ni muongo na huenda naye vilevile ni jipu humu ndani, anapaswa kutumbuliwa, kwa sababu Mheshimiwa Nape amedanganya hili Bunge. Alipokuja kutoa tamko la Serikali alisema kwamba hoja mojawapo muhimu ni kwa nini taarifa isirushwe na TBC ni gharama. Akaeleza wametafuta muda mzuri wa kuonesha ufanisi wa watu waangalie taarifa ya habari lakini waende kazini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama mwalimu, kama mtu mzima, kama mzalendo nikajaribu kufanya assessment ya kawaida kwamba kama unaonyesha kipindi cha Bunge saa kumi kasoro dakika ishirini na unataka kwa watu wa Dar es Salaam kwa mfano kule Ukonga, Msongola, Mbondole, Kibanda cha Maiti kule au Uwanja wa Nyani atoke ili awahi mjini kati ni lazima aamke saa kumi na moja, maana yake baada ya kumaliza kuangalia taarifa ya habari ambayo imeanza saa tano au saa nne ataoga saa kumi na moja anaanza safari huyu mtu lazima asinzie. Nikajiuliza hapa kuna kuna ufanisi! Hapa kuna ufanisi wa kazi? Nikalijua jibu hapana siyo kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, ninyi viongozi wa Bunge hili mmebariki hicho kitu kifanyike, ninyi mnakubali tuzunfumze hapa, mtu akiongea hapa leo, kuna miongozo imetolewa watu wathibitishe tunataka uongo wa Mheshimiwa Nape athibitishe kabla ya kuhitimisha hoja yake hapa, kwa nini amedanganya Bunge, kwa nini amedanganya Watanzania! Hoja ambazo wametoa siyo za kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mmemwambia Mheshimiwa Kubenea athibitishe mambo aliyozungumza, sasa ufanisi wa kazi unaoonekana hapa ni nini! Haya mambo lazima tuyajadili. Mimi ningekuwa na uwezo hii hotuba isingejadiliwa kwa sababu hili jambo tungekuwa na watu ambao hili Bunge siyo CCM wengi, hii Serikali tungeiangusha leo, tungepiga vote of no confidence. Kwa sababu jambo hili siyo jambo la Waitara, siyo jambo la UKAWA, siyo jambo la CHADEMA au la CCM ni jambo la Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, yupo Mwanasheria hapa na wapo wataalam mbalimbali wamebobea. Ukisoma Ibara ya 18 ni haki ya Watanzania, tukisema mmevunja Katiba mnakataa kwa nini? Mnataka tusemeje sasa? Kama kweli mna nia njema ya kufanya kazi Serikali hii hapa kazi tu tena kwa mara ya kwanza tumepata Rais ambaye ni mwanasayansi, mwalimu, mtaalam maana yake masomo yangu na Magufuli sawa sawa, kwa sababau yeye ameongezeka cheo amekuwa Rais, mimi Mbunge! (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tunafanana. Ameongeza degree ya pili ni mwalimu wa Hesabu na Kemia, ndiyo Rais wa kwanza wa Tanzania msomi, mwanasayansi, mwalimu. Walimu hatuongopi challenges, tutasema chochote ili mradi kuna fact. Kama kuna kazi inafanyika kwa nini mnaficha, kwa hiyo hilo jambo kwa kweli nimeumia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine kitendo cha Mheshimiwa Nape kuja hapa jana wametangaza anasema kuna Diamond ataburudisha sijui wapi, kutakuwa na mwanamuziki King Kiki jioni ya leo maana yake ni rushwa, hiyo ni rushwa! (Makofi)
Kwanza mnaposema mnabana matumizi mnaondoa starehe. Huyu King Kiki na wenzake gharama za nani zimemleta hapa, anapiga pale nani analipia hizo gharama? Wabunge wote ambao wataenda kwenye hiyo miziki ili kuunga mkono habari ya Mheshimiwa Nape maana yake mtakuwa mmekula rushwa na wote mlaaniwe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ninataka mnisaidie, Mheshimiwa Nape amezungumza, mimi nimesikia story, amezungumza habari ya ngoma na nini, nimeangalia kwenye matumizi. Tulimuita Mheshimiwa Naibu Waziri Mheshimiwa Anastazia Wambura, alikuja Dada yangu kwenye Kamati ya UKIMWI na masuala ya dawa ya kulevya. Ikaonyesha kwamba hawakutenga fedha kwa ajili ya michezo kwa maana ile UMISHUMTA, UMISETA hawakutenga fedha na wanasema hawana mpango huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimepitia hapa wanapozungumza, wamezungumza habari ya Samatta, hawa ni watu ambao wamejikuza wenyewe kama kuku wa kienyeji, mkakuta wamefanikiwa mnawapongeza sana, mnawapa sifa kubwa. Wapi mpango wa Serikali ya kuendeleza vijana, wapi mpango wa kuendeleza michezo shuleni? Kuna vipaji vinakufa pale! Hapa nimeona kwenye vote 6002 Youth Development Program ni zero zero tu! Nimeona kwenye vote 6004 kwenye Sports Youth Development, hakuna fedha ambayo imetengwa pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, wenyewe wanasema fedha ambazo zinatengwa na Kamati imezungumza ukweli hakuna kilichopelekwa sasa unazungumza habari gani hapa? Kwa hiyo sisi tukae hapa Bunge kila mwaka bajeti ikija, King Kiki, Diamond biashara inaisha si ndiyo? Hiyo biashara mtafanya wenyewe watu wa CCM sisi hatufanyi biashara hiyo bwana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine nataka mnisaidie hapa iwe very clear. Wako Wabunge wa CCM humu ambao wanapiga makofi sana, wanafikiri hii hoja ya habari ni ya kwetu. Mimi nitaomba leo Watanzania wajue wale ambao wanapiga makofi kwamba tv isioneshwe waonekane halafu muwe tayari twende kwenye Majimbo tukawaambie kwamba hiyo ndiyo biashara mnayoifanya humu ndani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunawaambia Rais amehasisha vizuri anawaambia Watanzania kila ukinunua kitu ulipe kodi, kama umelipa kodi upewe risiti, kama hujapewa udai. Hizo fedha zilizokusanywa hapa ndipo mahala pake kwa kuzipanga matumizi yake, hamtaki waone! Wananchi walipwe kodi, lakini mipango wasione! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa mmepunguza bajeti, leo tumejadili hapa bajeti ya Afya imepunguzwa kwa shilingi bilioni 18. Mimi naomba wako wataalam pale, yupo ndugu yangu Ayoub Ryoba amepewa TBC, hii TBC ambayo Mheshimiwa Nape amezungumza alifanya kazi nzuri amesema sehemu kubwa ilikuwa inaisemea Serikali, lakini taarifa rasmi ni kwamba TBC ilifanya kazi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu uliopita hiyo ndiyo bottom line.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mimi siungi mkono.