Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimshukuru sana na nimpongeze sana Mheshimiwa Nape Nnauye kwa jinsi alivyoanza vizuri katika Wizara yake, anaonesha ni jinsi gani anavyopenda michezo na jinsi gani anavyoiweza Wizara hii kwa sababu anaonekana kabisa kwamba anaitendea haki, Mheshimiwa kaka Nape tunakutia moyo, watu wasikuvunje moyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee sana naomba niongelee kuhusu suala la Miss Tanzania. Miss Tanzania ni kati ya sanaa inayoitangaza nchi yetu, ni kweli kwamba kulikuwa kuna madoa ambayo wanapaswa kurekebisha, wanatakiwa wayarekebishe, lakini Mheshimiwa Waziri unatakiwa ukae nao, wewe na Wizara yako kuweka sawa ili sanaa hii isipotee, waendelee kuonesha mashindano ya Miss Tanzania kwa sababu ni kati ya mashindano yanayoitangaza nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za wasanii ni kazi ambazo zinapaswa kutetewa sana na Waheshimiwa Wabunge na nchi kwa ujumla. Nchi za wenzetu sanaa ndiyo inayoleta uchumi wa nchi, kwa mfano Nigeria na nchi nyingine, sanaa ni kitu cha muhimu sana.
Kwa hiyo, tunatakiwa tuangalie wasanii kwa macho mawili au kwa macho ya mbele zaidi ili tuwape moyo wasanii wetu. Tuangalie kazi zao, tuangalie jinsi ya kutengeneza utaratibu ili jasho lao na kazi zao zionekane, wasiwe wanafanya kazi halafu watu wanatoka tu huko pembeni, wanapata pesa kutokana na jasho la wasanii. Namuomba sana Mheshimiwa Rais awaangalie wasanii hawa kwa macho ya huruma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba wasanii wa Tanzania wako chini sana, wanadharaulika sana ni kwa sababu hawana mtetezi. Mheshimiwa Waziri uliangalie sana hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee zaidi narudi kwenye suala la kuonesha matangazo ya Bunge live. Kuhusiana na suala la kuonesha matangazo ya Bunge live hii ilipelekea Wabunge tukawa (Wabunge waliopita) maana nisiseme tukawa sikuwepo kipindi hicho, mimi pia nilikuwa naagalia televisheni. Wabunge walikuwa wanakaa tu hapa kwenye tv wakiuza sura hapo! Hawaendi kufanya kazi majimboni mwao! Kwa hiyo, ni suala ambalo wananchi wanatakiwa waelewe, utaratibu huu umefanyika ili kuwarudisha Wabunge waende kufanya kazi majimboni mwao! Siyo wanang‟ang‟ania kuonekana kwenye tv! Wanataka waonekane ili iweje? Mkitaka muonekane nendeni mfanye kazi majimboni kwenu! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni utaratibu mbaya sana, Wabunge tunawadanganya wananchi kwa sababu wananchi hawajui. Sasa hivi mnaonekana majimboni kwani uwongo? Mnakwenda majimboni sasa hivi na mnatakiwa muende mkafanyekazi majimboni! Siyo mnadanganya wananchi waungane na ninyi wawa-support eti ooh, Serikali ya CCM, Serikali ya CCM haitaki muone maovu! Maovu mbona ninyi ni waovu kuliko mtu yeyote!
Mheshimiwa Naibu Spika, natamani hata kulia! Mnatutia aibu! Najisikia uchungu sana! Mnadanganya wananchi….
MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana ndugu zangu wananchi waliotuchagua waelewe kwamba huu utaratibu katika mazingira ya kawaida ni kweli, wanaweza wasielewe lakini waelewe kwamba sasa hivi Wabunge tunatakiwa turudi kwao kufanya kazi na tukae karibu nao wananchi, ndiyo maana na wananchi wanatakiwa na wao wafanye kazi zao watakuwa wanatuangalia kwenye tv baadaye. Utaratibu huu ni mzuri sana na utawafaidisha wananchi na kuwanufaisha, tutakwenda kila siku majimboni.
Mheshimiwa Naibu Spika, sina la zaidi ahsante sana na nashukuru sana.