Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na nampongeza Mheshimiwa Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Mahakama.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli naipongeza sana Seikali kwa kujenga Mahakama ya Temeke. Nilikuwa Mbunge wa vipindi vilivyopita nilikuwa nataka ikamilike sana kuhusu Mahakama ya Temeke, sasa tumepata Mahakama Maalum yenye kila kitu mpaka chumba cha kunyonyeshea Watoto, hongereni sana.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hayo Mahakama za Wilaya zote za Mkoa Dar es Salaam zimejengwa na ziko vizuri sana. Ombi langu naomba Serikali iangalie Mahakama ya Mwanzo Mbagala; hali ni mbaya Mbagala. Idadi ya watu Mbagala ni kubwa na mahitaji ni makubwa sana. Naomba Serikali iangalie sana Mbagala.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono na tumekuwa na mobile mahakama maeneo ya Chanika na zile za pembezoni, shukrani sana.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja.