Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii muhimu kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kujaalia neema na baraka Watanzania. Aidha naungana na Watanzania kuipongeza sana Serikali yetu inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wetu mpendwa kwa jinsi inavyotekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020/2025 na kutatua kero ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nitoe mchango wangu kupitia hotuba ya Wizara na Kamati ya Katiba na Sheria; kwanza Serikali iangalie matumizi sahihi ya maadhimisho ya siku ya sheria kwa ajili ya kupata picha ya upande wa wapokea huduma ili kutathmini kwani kwa sasa jamii na wapokea huduma hawajafahamu kikamilifu maudhui ya maadhimisho hayo, hivyo basi kutafutwe muundo mzuri wa siku hiyo kuwa na tija nzuri zaidi ili kuleta ufanisi wa utendaji kazi na jamii kuwa na imani kwa mahakama kama mhimili wa kutoa haki kwa wapokea huduma za jamii na matumizi sahihi ya media, redio na mitandao ya kijamii.

Mheshimiwa Spika, Serikali yetu itoe fedha za kujenga na kukarabati mahakama zote kongwe zilizojengwa toka enzi za kikoloni kwani kwa sasa hazifai kwa matumizi, mfano huo ni Mahakama ya Wilaya ya Mbulu, tunaomba sana Mheshimiwa Waziri atembelee na maeneo mengine nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali ijitahidi kutoa fedha zinazoombwa kwenye bajeti kwani hadi mwezi Februari, 2022 ni kiasi cha asilimia 29.87 kilichotolewa ya maombi ya matumizi, kiasi hiki ni kidogo sana kulingana na malengo yaliyotarajiwa katika kutekeleza majukumu yake muhimu na katika maombi ya miradi ya maendeleo hadi Februari, 2022 ni asilimia 45.37; hali hii itaathiri mpango wa bajeti ya maendeleo ya mwaka 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, Serikali iandae kalenda ya vikao vya Kamati ya Maadili za Wilaya na Mikoa na kuwepo kwa wajumbe kutoka upande wa wapokea huduma ili kupata taswira ya upande huu. Aidha, ni muhimu sana kuangalia hadidu za ajenda Kamati ya Maadili za Mahakama.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.