Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika hotuba hii kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanja vya michezo vimegeuzwa kuwa viwanja vya usheherekeaji wa sherehe mbalimbali na badala ya kuviendeleza kama viwanja vya michezo ambavyo vingeweza kuwasaidia vijana, wanawake na watoto katika kujenga, kufurahia kuimarisha afya zetu na kuchangamsha miili yetu na hata kutupa afya njema kila siku. Hatimaye viwanja hivyo vimegeuzwa kuwa sehemu ya kufanyia sherehe za Kitaifa na sherehe za Chama cha Mapinduzi (CCM). Mbaya zaidi viwanja hivi vimegeuzwa viwanja vya CCM, kwa sababu vyama vya upinzani hawaruhusiwi kufanya shughuli zao katika viwanja hivi isipokuwa Chama cha Mapinduzi tu. Nina ushahidi na hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Mheshimiwa Waziri atusaidie viwanja hivi vitumike kwa shughuli za michezo na kama ni shughuli nyingine basi kuwe na usawa na haki kwa sababu vyama au itikadi ni mapenzi ya mtu binafsi tu, lakini mwisho wa siku Utanzania wetu unabaki pale pale.