Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kilio cha wananchi wa Kakonko kutosikia chombo cha Taifa yaani TBC Redio. Hali hii hupelekea wananchi hao kusikiliza redio za nchi jirani kama Burundi na Rwanda, hivyo kukosa haki ya kujua nini kinaendelea nchini mwao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri ujengwe mtambo wa kuwawezesha kusikiliza redio yao ya Taifa (TBC), mtambo wa Kigoma Mjini uboreshwe ili usikike mkoa mzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kakonko haina Afisa Habari, Utamaduni na Michezo. Hali hii inawanyima vijana haki ya kupata fursa ya elimu juu ya utamaduni, sanaa na michezo kwa kukosa mtalaam huyo. Nashauri aajiriwe mtalaam huyo mapema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu viwanja vya michezo vilivyojengwa kwa nguvu za wananchi, baadaye vikachukuliwa na CCM. Viwanja vingi vina hali mbaya, havina hadhi ya kuendeshea michezo. Nashauri kwa nini visibinafsishwe kwa wadau wapenda michezo, vichukuliwe na Jeshi kama vile SUMA ili waviendeleze.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi ijipange kuandaa timu ya Taifa ambayo ina mrengo wa kucheza Kombe la Dunia, maandalizi haya yaanzie ngazi ya chini kwa vijana wadogo na ichukue muda hata miaka kumi kwa kuweka kwenye shule maalum (sport academy).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu motisha kwa wachezaji na wasanii hodari; Serikali iwe na utaratibu wa kutoa motisha kwa wachezaji hodari na wale wanaoileta sifa kwa nchi hii kama vile Ndugu Mbwana Samatta, Ndugu Francis Cheka na wengine. Mfano mzuri wa kuigwa ni wachezaji wa timu ya TP Mazembe ya Congo ilivyotwaa Kombe la Afrika, wachezaji wake walizawadiwa magari aina ya Prado tena mapya kila mchezaji. Hii pia ifanyike kwa wasanii wanaofanya vizuri nchi za nje kama vile Diamond, Mpoto na wengine.