Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia katika Wizara hii kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo la viwanja vya michezo kwa shule za msingi katika mji wa Njombe. Shule hizo ni shule ya msingi ya Mpechi, Sabasaba na Idundilanga katika Halmashauri ya Njombe Mji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shule hizo zilikuwa na viwanja ambavyo vimechukuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM). Naomba Waziri asaidie kutatua tatizo hilo ili viwanja hivyo virudi kwenye shule hizo waweze kufanya michezo kama ilivyokuwa huko nyuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.