Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri na uongozi wote wa Wizara na taasisi zake na wasanii wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sanaa za kazi za mikono na sanaa za ufundi zipewe msukumo zaidi ili kuwawezesha vijana wengi kutengeneza na kujifunza sanaa hizo ili waweze kujiajiri na kupunguza umaskini wa kipato pamoja na kuongeza Pato la Taifa. Maigizo na filamu zinazokiuka maadili ya Mtanzania zisiruhusiwe kuoneshwa katika jamii ili kupunguza mmomonyoko wa maadili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lugha ya Kiswahili ipewe msukumo zaidi ili Kiswahili kiweze kuwa ni mojawapo ya lugha yenye nguvu na iweze kuzungmzwa na nchi nyingi duniani. Hivyo itapelekea Watanzania kupata ajira zaidi katika kufundisha lugha ya Kiswahili. Pia Kiswahili kitaongeza umaarufu wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.