Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi hii ya kuchangia hoja iliyoletwa mbele yetu siku ya leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nianze kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji mzuri sana. Vilevile nimpongeze kwa kazi nzuri ambayo imekuwa ikifanywa na Wizara hii. Hii inadhihirisha kuwa Wizara imepata Waziri pamoja na Naibu Waziri walio makini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niende moja kwa moja, niunge mkono hoja iliyoletwa mbele yetu. Natambua kuwa Serikali yetu imefanya mambo mengi na inaendelea kuhakikisha kuwa utamaduni, sanaa na michezo inapewa kipaumblele hasa kwa vijana wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo ya msingi ningependa kuishauri Serikali. Kwanza tuhakikishe kwamba sanaa na michezo inapewa kipaumbele toka shule za msingi. Lazima tuhakikishe vijana wetu wanapewa vifaa vya michezo na sanaa. Shule nyingi hazina viwanja vizuri vya michezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuhakikishe tunawekeza kupata walimu wazuri wa kuwafundisha hawa vijana wetu. Lazima sisi kama Taifa tuhakikishe tuna academy kuibua vipaji vya vijana wetu katika michezo mbalimbali kama vile basketball, volleyball, mbio na sanaa kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo tutajihakikishia Taifa letu litakuwa na uhakika wa kuwa na vijana ambao wataweza kushindana na mataifa yaliyoendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.