Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo ni afya, michezo ni furaha, michezo huondoa mawazo na kadhalika, lakini hapa nchini hakuna viwanja vya michezo. Serikali ya Awamu ya Tano ilisisitiza sana suala la michezo. Je, mmejipangaje kuwapatia wananchi sehemu za kufanyia mazoezi? Kwa mfano katika Manispaa ya Moshi kila mwezi wa tatu tuna mashindano ya kimataifa yajulikanayo kama Kilimanjaro Marathon. Mbio hizi kwa sasa hivi zina washiriki zaidi ya milioni 10 kutoka mataifa mbalimbali lakini tumekuwa tukitumia uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi (MUCOBS) ambacho kwa sasa kinalemewa na wingi wa washiriki wa mbio hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Manispaa ya Moshi tunao uwanja mkubwa wa King George Memorial Stadium ambao kwa sasa unatumika kama soko la kuuzia mitumba. Moshi kuna sehemu nyingi za masoko mfano Pasua, Majengo, Manyema na kadhalika ambako soko hili linaweza kuhamishiwa huko na uwanja wa King George Memorial Stadium ukatumika kwa ajili ya michezo, ukizingatia uwanja ule una michezo tofauti zaidi ya saba. Ni tegemeo langu Serikali itatoa tamko kuhusu kiwanja hiki ili tuweze kudumisha michezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuwepo Maafisa Utamaduni lakini bado hawajaweza kutumika ipasavyo katika kukuza utamaduni wetu. Kwa mfano, cultural tourism haijapata msukumo wa kutosha kutoka kwa maafisa hawa. Urithi wetu unaelekea kupotea kwa mfano, ngoma za asili, vyakula vya asili, michezo ya asili, mavazi ya asili hata lugha za asili. Hii ni changamoto kubwa kwa Maafisa Utamaduni hasa ukizingatia tishio la utandawazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kuwa Maafisa Utamaduni wawezeshwe kwa kupewa rasilimali za kutosha ikiwa ni pamoja na vitendea kazi ili waweze kuwafikia walengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, mchakato wa Vazi la Taifa umefikia wapi na mpaka sasa hivi ni kiasi gani cha fedha kilichotumika?