Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru sana kwa kuruhusu niletewe maji hapa juu ya meza kwa sababu nakohoa sana. Nisingesema haya, najua ningepigwa Mwongozo sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja na vilevile kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kuwasilisha hotuba yao kwa ufasaha mkubwa. Niongelee kwa kifupi sana kilio cha maslahi ya wasanii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kuingilia maudhui ya mashauri ambayo yako mahakamani sasa hivi, mimi naona mabadiliko makubwa sana na ya kutia moyo katika mentality ya vijana wetu sasa hivi. Vijana wetu sasa hivi wanathubutu, wanakwenda mahakamani, wanaachana na tabia iliyoanza kujengeka hapa ya kutunga ngonjera za kulalamika tu, ni kulalamika na kutegemea kila kitu wafanyiwe na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetunga Sheria ya Hatimiliki mwaka 1999. Nashukuru Mungu kwamba mimi nilihusika kama mtaalam, nilihusika kuiunda COSOTA vilevile; na nilikuwa Mjumbe wa kwanza wa COSOTA; na vilevile nilihusika kuanzisha kozi ya Intellectual Property Law, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na yote hii ni kutetea wasanii wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kipindi hicho tulikuwa tunabezwa, kwamba aah, alinacha hiyo. Wengine waliotubeza walikuwa wasanii, lakini walikuwa hawaelewi. Vilevile tuliungwa mkono na nguli wa muziki kama akina Hamza Kalala, akina King Kiki (Kikumbi Mwanza) na leo jioni tuko naye na kitambaa cheupe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachosema tu ni kwamba nafurahi vijana wanapokwenda mahakamani to battle for their rights. Sheria hatutungi ziwekwe kabatini, zinatungwa ziweze kutumika na vijana na hii inatufurahisha. Hata mwanasayansi nguli, Newton aliwahi kusema; “an object at rest will always remain at rest unless acted upon.” Kwa hiyo, vijana tayari tumewawekea mazingira, tuna sheria. Ile sheria ni nzuri tu, piganieni haki zenu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimkumbushe pia Mheshimiwa Ahmed Ngwali, ameongelea kidogo kuhusu sheria moja kwenye michezo, kwamba Waziri unafanya nini? Hapana! Mheshimiwa Ngwali, basi wewe hujaelewa unafanya nini hapa. Siyo kazi ya Waziri wa Katiba na Sheria kuzunguka nchi nzima kusema sheria hii inawafaa au la! Ni stakeholders. Ni ninyi wenyewe mnaotumia sheria hiyo kusema sheria hii sasa imepitwa na muda; kama ulivyofanya sasa hivi, na wewe ni Mbunge, ilete Bungeni. Sio Waziri wa Sheria aende Ibadakuli, aende sijui Mtwara aulize hii sheria inawafaa au laa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu nigusie haraka haraka sana kwa sababu muda wenyewe ni mdogo, mambo mawili matatu ambayo yameongelewa na Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni. Ukisoma hotuba yake ukurasa wa pili, wa tatu na wa nne Mheshimiwa Mbilinyi anaonesha kuamini kabisa kuwa uhuru wa kutafuta, kupata na kusambaza habari ni absolute, ni uhuru unaotakiwa usiwe na mipaka kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mipaka yoyote ikionekana kwenye tasnia hii, basi huo ni udikteta. Hapana Mheshimiwa, hapana kabisa. Katika dunia hii, hakuna uhuru wala haki isiyo na mipaka. Sijawahi kuona. Hakuna nchi iliyofungulia milango kila kitu. Kama nchi hiyo ipo, nakuhakikishia Mheshimiwa Waziri Kivuli, mimi nitachangisha fedha tukuhamishie huko. Hakuna! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuomba usome tu Ibara moja maarufu inaitwa Artcle 19. Waandishi wa Habari wote wanaifahamu. Kwasababu, Article 19 ambayo iko kwenye Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa, ndiyo inayoweka msingi wa haki hiyo Kikatiba duniani kote. Ilipitishwa na Umoja wa Mataifa. Article 19 loh, sasa sijui utaniruhusu Mheshimiwa nisome…
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Nimemwomba Mwenyekiti, siyo ninyi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Article 19 inasema: “Everyone shall have the right to freedom of expression. This right shall include freedom to seek, receive and impart information and the ideas of all kinds” bila kuingiliwa. Unahakikishiwa kupata habari, usiingiliwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini article hiyo hiyo inakuja kwenye clause (3); “The exercise of the rights provided for in paragraph two above, carries with it special duties and responsibilities,” yaani wajibu na majukumu maalum. Hupewi tu haki na kuachiwa nenda kaogelee. Hilo tulikubali dunia nzima. It may therefore be subject to certain restrictions, yaani masharti maalum. But these shall only be such as are provided by law; na sisi kama tulivyofanya Tanzania, tume-provide by law for respect of the rights or reputation of others;” kwa heshima ya watu wengine na haki za watu wengine. Vilevile inasema kwa kulinda usalama wa Taifa lako mwenyewe. Kwa hiyo, hakuna uhuru usio na mipaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona wengi hapa wanatoa mifano ya nchi nyingi zenye uhuru usio na mipaka, wa ajabu sana. Marekani ndiyo inasemekana kwamba ina uhuru usio na mipaka, hapana. Marekani pia ina-enjoy privileges chini ya Article 19, lakini vilevile Marekani ni nchi ambayo ime-retain Sheria mbovu kweli kweli za kubana vyombo vya habari kwa miaka zaidi ya 239. Sheria zenyewe ni kwanza Press Law/Press Code yao ni Cap. 115 kitu kama hicho. Vile vile wana Sheria ya Alien and Sedition Act iliyotungwa mwaka 1789. Wewe andika kitu ambacho kina-threaten stability ya Marekani, halafu uje usimulie kuhusu uhuru huo wa Marekani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka tu niseme kwamba Mheshimiwa Waziri Kivuli kwa kweli ameichora kwenye hotuba yake hii nchi yetu kama ni ya kidikiteta hivi; mimi nauliza tu Mheshimiwa Waziri Kivuli, hii nchi ingekuwa ya kidikiteta, ungeweza kweli ukafyatuka jinsi unavyofyatuka hapa? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Waziri Kivuli amenukuu tafiti nyingi sana, lakini mimi nafahamu kwa watu wengi ambao wako katika hii tasnia kuna reliable data. Kwa mfano, Press Freedom Index ambayo inachangiwa na taasisi nyingi za Kimataifa. Ile press index, mimi nimeangalia mwaka 2014, 2015 na 2016, inatoka kila mwaka, imetaja nchi 20 duniani ambazo zina hali mbaya ya vyombo vya habari na utoaji haki kwa wanahabari, Tanzania haimo. Imetoa orodha ya nchi kumi ambazo hali ni mbaya kupita kiasi, Tanzania haimo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo madai ya kwamba kuna ukiukwaji wa Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninayo hapa, hii ni kutokana na uamuzi wa Bunge kuwa na studio yake na kurusha matangazo pale. Mimi naomba kwa haraka tu nisome Ibara ya 18. Inasema: “Kila mtu:-
(b) anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari bila ya kujali mipaka ya nchi.” Imeiga kabisa ile Article 19!
“(d) anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu ya jamii.” (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapewa haki ya kutafuta, kupokea, kusambaza habari hapa, kusambaza taarifa, lakini Katiba hii haisemi hizo habari lazima ziwe live. Sijaiona hapa! (Makofi/Kicheko)
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA:Mheshimiwa Mwenyekiti, naongea kama mwanasheria, naomba… (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba…
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiendelea na tabia hii, hili siyo Bunge tena! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiendelea hivi hili siyo Bunge tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Ibara ya 18; there is no canon of constitutional interpretation itakuletea neno live hapa. Ninachosema, tusichanganye vitu viwili hapa, matakwa ya Kikatiba na matakwa ya kisiasa, ambayo yote ni muhimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu anakuja anasimama hapa anasema wananchi wanataka live. Wewe unawafikiria wananchi wapi? Wanaocheza pool ama wakulima ambao ni asilimia 80 ya Watanzania ambao asubuhi wanakuwa mashambani? Unaposema wananchi wanataka wakuone saa 4.00… (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaniongezea muda mrefu tu, kwa sababu huu upuuzi, siwezi…
(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila mpangilio)
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakimaliza kuongea, naomba uniambie niendelee.
MWENYEKITI: Naomba uendelee Mheshimiwa. Mheshimiwa naomba uendelee, jamani tufanye ndani ya muda…
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Meshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Dakika tano, nafikiri umeziona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, unaposema wananchi wanataka live, wananchi ambao leo ndiyo Taifa la leo na kesho ni wanafunzi wako vyuo vikuu, sekondari, wako darasani saa hizo!
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii the most popular program katika televisheni ni taarifa za habari. Taarifa za habari zote duniani ni mixture ya live na recorded programs. Nafikiri Bunge letu nalo limeiga huko huko, ni mixture ya live na recorded programs. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, namheshimu sana Mheshimiwa Devotha, alisema Mheshimiwa Waziri wa Habari alisema gharama ya live ni shilingi bilioni nne; hakusema kweli, kwani gharama ni shilingi bilioni mbili tu! Nikasema ehee ehee ehee, jamani! Serikali ya Awamu ya Tano, hata senti tano, it matters to us. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, shilingi bilioni mbili hizo, zitajenga matundu mangapi ya choo? Zitajenga shule ngapi? Zitajenga barabara ngapi? Leo kwa sababu ya mahitaji ya kisiasa uonekane live. Tena mimi namshukuru Mungu, nasema kwa aibu inayotokea hapa, mizozo mizozo isiyo ya msingi, ingekuwa live hapa, wengi wasingerudi hapa. (Makofi)
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Nkamia. Anasema jamani sisi ni Wabunge, let us think outside the box. Ametuletea mifano ya BBC, ametuongelea kuhusu masuala ya tv license yanayoifanya BBC iendelee, siyo hii TBC yetu ambayo inalia njaa na bajeti yake wenyewe mnalalamikia hapa. Hiyo ndiyo kazi yetu sisi kama Wabunge, siyo kudai tu kama watoto wadogo, nataka uji, nataka uji, uji umeutolea hela?
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Tunaambiwa, live imezuiwa kwa sababu CCM wanaogopa madudu, jamani… (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, let us be fair to ourselves. Mimi nadhani hata kukatisha hizi live programs tumewapendelea sana Upinzani.
(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila mpangilio)
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii ingekuwa kila siku wananchi wanayasikia mambo ambayo Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Dkt. Pombe Magufuli inayofanya mambo makubwa nchi hii, upinzani hawana nafasi kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kelele hizi za yeehee, yeehee, yote ni kukosa hoja. Kwa hiyo, ni kupiga kelele tu kama watoto wadogo.
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Nape Nnauye na mwenzako, mmetoa bajeti nzuri, tutawalinda na tutaipitisha! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.