Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. TOUFIQ SALIM TURKY: Mhehsimiwa Spika, ahsante. Awali ya yote naomba tumshukuru Mwenyezi Mungu subhanahu wa ta’ala kwa kutujalia kufika siku ya leo nikiambatana na familia kwa mara ya kwanza pia nikiwa na mke. Wengi wanasema ametoka Uhindini lakini ni Mturuki, kwa hiyo nimetafuta asili kidogo. Pia naomba tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia mfungo huu wa Ramadhan umefika kwa salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kweli katuheshimisha sana ndani ya Tanzania yetu na nje ya Tanzania yetu. Kwa kipindi kifupi mno, na hususan wengi tukiamini akina mama speed zao zinakuwa ndogo, lakini kusema kweli wengi wetu katufunulia macho yetu na kudhihirisha kuwa mama anafanya kazi kubwa mno, katika nyanja zote. Kama tukiongelea kilimo basi kulikuwa kuna mapinduzi ya kilimo nafikiri sote mashahidi; tukijaa katika suala la zahanati, sasa hivi kila Wilaya sasa hivi inaongelea masuala ya zahanati, shule, maji, umeme.

Mhehsimiwa Spika, nilikuwa katika Bunge la Afrika ya kule South Africa, wenzetu wana mgao wa umeme wa masaa sita, hakuna umeme ni bara linasemekana kuwa la kwanza ndani ya Afrika na wapo katika G-20 hawana umeme, South Africa, lakini Tanzania tuna umeme. Sasa ni muhimu sana tukawa watu tunaongelea mengi tu. Najua bado hatujafikia kiwango kikubwa tunachokitaka lakini kazi tunafanya. Kwa hivyo ni muhimu sana linapokuja wakati wa kupongezana ni muhimu kutoa hiyo taarifa. Si umeme tu; lakini nitashangazwa; tulikuwa katika mall fulani kule Johannesburg katika mji mkuu kabisa basi ndani ya lile mall kulikosekana maji. Sidhani kama tumeenda sisi sehemu hapa zetu kuu tukakosa maji, nafikiri tunapaswa pakubwa sana kumpongeza Mama yetu kwa namna kazi namna anavyochapa kazi.

Mheshimiwa Spika, hali kadhalika tumeona katika Bahari, hususan katika maziwa tuna MV Mwanza sahivi, ni meli ya namna yake ambayo imejengwa kwa kuhakikisha katika maziwa yetu masuala ya safari, mizigo yanaenda salama na uchumi unaweza kuimarika. Lakini pia mwenzangu hapa alikuwepo Bw. Tabasamu akaniambia daraja lake la Kigongo limeshakamilika, limebakia nguzo tatu tu na mkandarasi ashalipwa kila kila kitu. Kwa hivyo hapo tunatakiwa tumpongeze mno.

Mheshimiwa Spika, na mimi katika hoja hii ya kumchangia Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba nimpongeze sana kwa hotuba yake ya jana. Amegusa sehemu zote, nafikiri Watanzania tuliosikiliza imeigusa kila mwana Tanzania; na tumeona namna gani Serikali ya Mama na hususan kupitia Mhehsimiwa Waziri Mkuu, namna walivyojipanga kuhakikisha umasikini unazidi kupungua na watu wanapata faraja ndani ya Tanzania yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii nilitaka kuchangia hoja moja tu, na mara nyingi napenda kuichangia hiyo kwa sababu watu wameona kama ipo mbali sana lakini hili suala haliko mbali bali lishafika.

Mheshimiwa Spika, wakati wa zamani uchumi ulivyoanza wakulima walikuwa wanatumia mikono. Zilipokuja mashine wengi wao wakaona kazi inaanza kupungua zinaenda kwenye mashime sasa sisi hatutafanya kazi, ajira. Ikaja wakati sasa wakaona kumbe sio kwamba tutapungukiwa lakini ile work force ikahama ikaenda katika industrialization; kwenye viwanda, kwa kuwasaidia karakana zile mashime ziweze kujengwa. Ikaja wakati wa 80 dunia ikapatwa na janga kubwa, ajira zikashuka kwa sababu yaliingia masuala ya kompyuta na watu wengi sana wakakosa zile ajira kwa sababu watu walikuwa wameshazoea ma-typewriter kuandika barua na nini yote yakachukuliwa katika work force ikaenda katika kompyuta, watu wakaona kazi zitakosekana. Ni kweli zilikosekana zikachukua muda, lakini baada ya hapo watu wakapata kazi na dunia ikaendelea.

Mheshimiwa Spika, nimesoma majarida mbalimbali na imefanyiwa tathmini; kwamba, miaka mitano mpaka kumi ijayo takriban robo ya Europe na Marekani, robo ya work force itakuja kuondoka, inaondoka wapi? Kuna kitu kinaitwa Artificial Intelligence; ambapo kuna wahariri, waandishi wa habari humo ma-journalist waliozoea kuandika vitabu majalada, matoleo mabalimbali na newspaper; hata watu wetu wa hansard hizo kazi zitaenda kwenye a high; ni mfumo, zinaenda kwenye mfumo watu hawahitajiki tena.

Mheshimiwa Spika, kuna kazi za utawala za kupeleka barua sijui za administrative work; zote zile zitapungua. Kazi za sheria, kuandika sijui mabarua ya kupeleka kisheria, kuandika zile code kila kitu nyingi zitapungua; hali kadhalika katika masuala ya ujenzi, mawasiliano na maitnaince. Hili sio kama litakuja tayari limeanza.

Mheshimiwa Spika, jana, kwa bahati, kuna App niliisoma; na naombeni Waheshimiwa Wabunge na nyie mkipata nafasi mnaweza mkai-download inaitwa Chat-GPT. Hii Chat-GPT umei-download unamwambia nataka nimuandikie barua Waziri Mkuu nimuelezee nina changamoto a b c basi, inaandika barua, tena unamwambia niandikie kwa namna ya shakespeare inakuandikia kila kitu na tena kwa namna ya literature unayoitaka wewe. Maana yake nini kama mtu ulikuwa hujui kuandika, hujasoma sijui hujafanya nini, yote inafanya yenyewe. Sasa tujiulize wale watu waliokuwa wanafanya watapata wapi kazi hizo? Hata hivyo, sasa tunatakiwa na sisi tuwe na think tank yetu ambayo sasa humu ndani na naomba tuishauri Serikali kuwa na think tank ambayo itaweza kutathmini na sisi tutaathirika vipi katika hili wimbi jipya lililokuja duniani la artificial intelligence. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfano mdogo ni suala zima la madereva, kama tunavyokumbuka zamani madereva walikuwa unaenda zako sehemu mbalimbali wanakusimamisha njia, lakini sasa hivi una bolt, bolt ile imesababisha mtu yeyote anaweza kujiajiri, lakini wale madereva wa zamani sasa hivi wamepungukiwa na kazi kwa sababu, sasa hivi hutaki kujua akili yako. Kwa hivyo, naishauri Serikali kuwa na kamati, la kwanza kuwa na semina ya Wabunge humu ndani tufahamu nini artificial intelligence, ili tuweze kuwasaidia wenzetu wengi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. TOUFIQ SALIM TURKY: Mheshimiwa Spika, nashukuru na naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)