Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa hii leo tena.

Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa hotuba nzuri ambayo Waziri Mkuu ameisoma jana ambayo imesheheni matumaini makubwa, lakini hoja yangu leo itakuwa ni umuhimu wa binadamu kutoa fursa kwa binadamu mwingine kuishi.

Mheshimiwa Spika, upo ukatili unaendelea juu ya binadamu na sisi tusipokuwa makini specie yetu kama viumbe hai kama binadamu tunakwenda kupotea.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu amesema jana namna ambavyo Serikali imetekeleza mambo yake kwa mwaka ulioisha na fedha nyingi tulizowekeza huko, zaidi ya trilioni nane kwa ajili ya kutengeneza miundombinu mbalimbali ya kuhakikisha kwamba, ustawi wa binadamu katika nchi yetu unaendelea kuwepo. Naamini kabisa fedha nyingi tunazowekeza kwenye miradi ya kimkakati nia na madhumuni yake sio kutusaidia sisi tunaoishi leo peke yetu, tuna nia ya kuwasaidia watoto wetu, tuna nia ya kuwasaidia wajukuu zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumewekeza zaidi ya bilioni 762 kwenye reli ambayo tunategemea itaishi zaidi ya miaka 100 ijayo na yamkini sisi katika miaka 100 ijayo sisi hatutakuwepo. Tumewekeza katika bwawa la umeme zaidi ya bilioni 800, Bwawa la Mwalimu Nyerere, hatutakuwepo. Tunawekeza katika miundombinu ya viwanja vya ndege zaidi ya bilioni 77 na Iringa tumepata bilioni 41 kwa ajili ya kujenga Kiwanja cha Nduli, kimefika asilimia 42 lakini tunajua tuliambiwa mpaka Septemba kitakuwa kimekamilika, tunajua zitaletwa fedha, lakini nia na madhumuni ni kwamba, tusaidie watoto wetu na wajukuu zetu na vizazi vijavyo, kama Watanzania na Waafrika.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu ameeleza mipango ya maliasili za Taifa letu, jinsi tunavyotaka kuendelea kulinda maliasili zetu sio kwa ajili yetu sisi tu, kwa ajili ya watoto wetu na uzao ujao. Mama alivyojitolea kwa ajili ya kufanya ile movie ya Royal Tour, nia na madhumuni sio ataiona yeye peke yake na Awamu yake ya Sita, nia na madhumuni wajukuu wetu pia waje waione.

Mheshimiwa Spika, yapo mambo yanayoendelea katika jamii yetu. Tusipokuwa makini na tukienda kwa ku-copy na ku-paste kwa sababu, watu fulani wamesema au mataifa fulani yamesema, sisi tusipoamua kutumia akili zetu na kwamba, tumepewa fursa na Mungu na sisi kama Watanzania kuamua mambo yetu, upo wakati na sisi kama Watanzania tutoe fursa mataifa mengine yaje yajifunze kutoka kwetu namna ambavyo tunalea watoto wetu, namna ambavyo tunakuza watoto wetu.

Mheshimiwa Spika, sisi kama Waafrika hatukufundishwa kujifunza tu kwa watu wengine. Afterall Mungu aliumba mtu mke na mume hakuangalia color ilikuwa ni color gani, kwa hiyo, na sisi watu wengine, mataifa mengine wanatakiwa waje wajifunze namna ambavyo Afrika inatunza watoto wake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa katikati ukatili kwa watoto wetu umezidi mno. Tunashangaa, hatuelewi imetokea wapi? Imekuwaje? Waziri Mkuu ameeleza hali ya usalama wa nchi yetu na utulivu iko vizuri, mipaka yetu iko vizuri na ni kweli, wote tunashuhudia tuko vizuri, lakini kumbe ndani ya nchi kwenye uzao wetu tayari hatuko salama. Watoto wetu wamefanyiwa vitu vya hovyo mno. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo kumbe humu ndani tuna taasisi, tena Mheshimiwa Waziri Mkuu katika ku-wind up hotuba yake ameeleza mambo muhimu ambayo anataka yafuatwe. Moja katika yale sita, ameeleza jambo la tatu anasema, viongozi wetu wa Serikali, dini, mil ana vyama vya siasa wakemee kwa nguvu zote ushiriki wa sehemu yoyote ya jamii katika matendo yasiyoendana na mila, tamaduni na desturi za Watanzania. Hii ni pamoja na wazazi na walezi wote kushiriki kikamilifu katika makuzi na malezi bora ya watoto yatakayosaidia kuwaepusha na vitendo viovu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, it is a high time suala hili linalohusiana na ukatili kwa watoto wetu, ulawiti kwa watoto wetu, ubakaji kwa watoto wetu, masuala ya ndoa za jinsia moja yasifumbiwe macho. Tuyaongelee Makanisani, tuyaongelee Misikitini, tunaanza hapa Bungeni, tuyaongelee Serikalini, tuyaongelee kwenye familia zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tutapotea. Hizi reli zitakuja kupandwa na popo kama ilivyokuwa Sodoma na Gomora. Huu umeme hautakuwa na maana. Haya majengo makubwa tunayojenga hayatakuwa na maana. Barabara ile wanayotujengea Iringa kwenda Ruaha National Park nani atapanda nani ataangalia wale tembo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimesema lazima binadamu mmoja atoe fursa kwa binadamu mwingine. Kama babu yangu mimi asingetoa fursa kwa baba yangu mimi leo ningekuwa wapi? Angemua babu yangu mimi aolewe na babu mwingine wa Kijiji kile ingekuwaje? Mimi leo ningekuwa wapi? Kama mama yangu angeona ndoa zina shida akaamua kuolewa na mwanamke mwingine, mimi leo ningekuwa wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lazima vijana wetu waambiwe ukweli. Sisi tunawapenda, tunawaheshimu ndio maana tunawekeza, ndio maana mama hakawii anazunguka huko na huko kwa sababu ya kuhakikisha kwamba, tunalinda Watanzania na uzao wao. Sasa leo tukikaa kimya kwa sababu, ni human right, ni human right ipi wakati sisi hatutoi fursa? Sisi tulipewa right ya kuishi na moja among the human rights ni haki ya mtu kuishi na wewe unatakiwa kutoa fursa kwa mtu mwingine aishi, you don’t give the right halafu unataka upewe right, haiwezekani! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, twende kwenye shule zetu na si suala tu la Serikali kusema kwamba, sasa Serikali ije hapa maendeleo ya jamii watwambie hiyo jamii wanayoitunza ni ipi? Hii mipango tunayoitenga ya nini? Haya mabilioni ya fedha tunayaweka ya nini kama hayataangalia uzao wa tumbo letu? Kama hatutaangalia watoto wetu wanaishi vipi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo watoto wako kwenye vulgar environment, hawaelewi waende wapi. Wakija majumbani tafiti za UN zinaonesha kwamba, 66% ya watoto wanafanyiwa ukatili majumbani kwa wazazi wao, 44% inayobaki ni shuleni na sehemu nyingine. Wanakwenda shuleni tena wale guardians ambao tumewakabidhi watoto nao tena wanawalawiti watoto, wanawafanyia ubakaji watoto. Tanzania where is this country heading to? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi we need to be a role modal in this world. Other people should come also and learn from Tanzania kwamba na sisi tumeweza kuwa-groom watoto wetu, sio lazima tuige kila kitu from them. Hata wao wenyewe wame-confuse. Nimemsikia Biden mwenyewe anasema, anashangaa anasema my mum alisema tu it is sinful, halafu akasema it is cruelty kwa binadamu, ni ukatili kwa binadamu. Wenyewe hawaelewi, yaani they don’t know what to say. They find somewhere to read, wanataka mahali wakajifunze. Tanzania we are ready, tulikuwa tuna-raise vipi watoto wetu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo Japani wanahangaika kwamba, uzao wao unakwisha kwa sababu, mwanamke ana uwezo wa kuzaa mtoto 1.3 kwa sisi tuliosoma hesabu maana yake kati ya wanawake wanne anayezaa watoto wawili ni mmoja tu. Wengine wanazaa mmoja wengine labda hawazai. Watu wanaona population yao inashuka, they are fighting, Waziri Mkuu yule ana-fight namna gani ainue population yake. Sasa kama it is a human right wao kuoana wanawake kwa wanawake na wanaume kwa wanaume kwa nini wanawa- force watoto wetu waingie kwenye hizo kwa kuwalazimisha kufanya vitu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wao nao wa-grow wafike waamue wenyewe. Nashindwa kuelewa NGO ndani ya nchi hii. Nimerudi Iringa nimekutana na hiyo, vijana wananiambia kuna mahali mmetupeleka tukafundishwe tukopeshwe, lakini madam mbona kama vile wanatufundisha mambo fulani? In this country! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumewaruhusu, halafu hiyohiyo Wizara ya Maendeleo ya jamii, hiyo hiyo ndio inasajili NGO, hiyo hiyo ndio inatakiwa kulinda jamii, hiyo hiyo ndio inatuletea watu wanagawa vilainishi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, look here, we are privileged to be leaders in this country. Ni neema, it is a grace. Tusije tukajiona kwamba, sisi ni wa maana sana kuliko watu wengine, we are graced na tusipotumia neema hii vizuri, leo tukikaa kimya Mungu atainua mawe yatasema, ila sisi na uzao wetu utapotea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, narudia tena, binadamu atoe fursa ya binadamu mwingine kuishi. We love them, they are our kids. Ni watoto wetu, tunawapenda, hata hawa walioingia kwenye mifumo hiyo ya ndoa za jinsia moja au ushoga hatuwachukii ni watoto wetu, mtoto wako hata akiwa kibaka utamkataa?

Mheshimiwa Spika, tutafute mbinu za kuwasaidia wale watoto wetu. Tuone namna gani tutakaa, kama we think kwamba, dunia ime-advance scientifically let that science prove kwamba, inaweza ku-solve problems kama hizi. Science ituhakikishie kama inaweza kumsaidia kijana wetu wa kiume aliye-engage huko, amepoteza kabisa viungo vyake, nguvu zake hazi-function, itusaidie. Hatujamaliza bado kupambana na matatizo ya uzazi wa wanawake, leo tuanze kupambana na kubadilisha matumbo ya wanaume yawe ya akinamama, inawezekanaje? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya tu ambayo ni original tumepewa bure tumeshindwa kuyashughulikia…

SPIKA: Mheshimiwa Jesca Msambatavangu muda wako umeisha. Dakika moja, malizia.

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame kwa pamoja. Kwa agizo hili twende kwa pamoja, ukisimama hapa wekaweka kidogo mbwembwe, haiwezekani, Ubunge wetu hauna maana kama watoto wetu hawatakuwepo baada ya miaka 10. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hatuko tayari kuacha Tanzania iwe ni nchi kama ilivyo Sodoma na Gomora wanazaliana popo. We are not ready, we are here ku-make sure Watanzania wanaendelea kuwepo katika ulimwengu huu mpaka ukamilifu wa dahari, ahsante. (Makofi)