Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi hii kwa siku ya leo niweze kuchangia taarifa iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu ndani ya Bunge letu. Kwanza binafsi nipende kupongeza Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kazi nzuri ambazo imekuwa ikiendeleza kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi hizi haziende bure, Mama samia ameonyesha kweli ni Mama jasiri, Mama shupavu, jemedari, Mama Hangaya, Mama kweli kweli kama kuna watu walikuwa wakidhani labda wanamjaribu Mama hajaribiwi na hili limedhihirika katika miaka yake miwili aliofanya kazi. Sisi kama Wabunge ni mashahidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeweza kuwa na miradi mikubwa kama Taifa, tuna mradi mkubwa wa Bwawa la Mwalimu Nyerere kuna mradi mkubwa wa ujenzi wa SGR, lakini pia kuna miradi ya ununuzi wa ndege na viwanja wa ndege, tuna ujenzi wa REA, vyote hivi amevikuta na amevipokea vikiwa katika asilimia ya chini lakini Mama huyu jasiri, shupavu, amesimama imara na kuonyesha dunia au kuonyesha Watanzania kwamba wakina mama wanaweza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bwawa la Mwalimu Nyerere wakati Mheshimiwa Rais anachukua nchi, bwawa hili lilikuwa limefikia asilimia 42 toka ujenzi wake uanze, lakini leo hii tunazungumza bwawa hili limeshafikia asilimia 83, maana yake zaidi ya nusu ya kazi imeshafanyika. Hata ujazo wa maji, maji yanayohitajika pale inatakiwa maji mita 164, mpaka leo tunazungumza kuna ujazo wa maji mita 134 maana yake kama hali ya hewa ikienda vizuri na mvua ikaja tuna hakika mita 29 zilizobakia tunaweza tukazipata na tukaanza majaribio ya umeme kutokana na bwawa lile la Mwalimu Julius Nyerere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bwawa hili linaenda kuongeza umeme kwenye gridi ya Taifa kuwa na umeme megawatt 2115. Kwa hiyo, ni kazi nzuri ambazo ameendeleza kuzifanya, ambapo watu wengine walidhani kwamba bwawa lile lisingeweza kufika mwisho. Tunampongeza na kumtia moyo Mheshimiwa Rais kwamba aendelee kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kubwa ambalo ameendelea kulifanya ni ujenzi wa reli. Tumeweza kuona ujenzi wa reli kutoka Dar es Salaam - Morogoro umeshafikia asilimia 97. Ujenzi wa reli ya Morogoro kuja Makutupora umeshafikia asilimia 92. Hii ni kazi nzuri na kubwa na ni kazi za kupongezwa, hizi kazi zimefikia asilimia hizi fedha zimelipwa, maana yake kazi zinazofuata zitakapokuwa zinaletwa certificate tunaweza kumalizia fedha zingine lakini kwa hizi kazi zinazofanyika hatudaiwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tumeona kazi ya ujenzi wa reli kutoka Makutupora kwenda Tabora asilimia nne tayari, tumeona ujenzi wa treni ya umeme kutoka Mwanza kuja Isaka umeshafikia asilimia 25, kwamba kazi inaendelea na tunampongeza sana Mheshimiwa Rais aendelee kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ameendelea kulifanya Mheshimiwa Rais ni ununuzi wa Ndege na ujenzi wa viwanja vya ndege. Hivi karibuni tutapokea ndege zingine Tano ikiwemo moja kubwa ya kubeba mizigo. Ninampongeza sana Mheshimiwa Rais, Wabunge tunaedelea kumuunga mkono na kumtia moyo kwamba aendelee kuchapa kazi. Mama anaupiga mwingi kweli kweli. Kwa wapenzi wa mpira tunasema Mama anaupiga kama Mayele vile, anaupiga kama Mayele maana yake sasa hivi Mayele ni maarufu duniani, ni maarufu Afrika kwa sababu jinsi anavyoweza kutupia magoli, ndivyo Mama anavyoweza kufanya kazi nzuri kwa Taifa letu. Tunampongeza sana Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anazozifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tusiishie hapo, ameweza kutoa fedha nyingi za barabara wewe ni shahidi.

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Mabula. Ahaa muda umekwisha.

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, muda umenipa dakika tano bado.

MWENYEKITI: Muda umeisha Mheshimiwa.

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ahsante.