Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwa heshima na taadhima nakushuru kwa kunipa nafasi. Waheshimiwa Wabunge na ndugu zangu Watanzania ambao tutapata fursa ya kulisikiliza Bunge letu, nina mambo ya msingi mawili ya kuyazungumza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ieleweke kwamba tunaposema kitu kinachoitwa Serikali lazima tujue ya kwamba wajibu na kazi ya Serikali ni kuhakikisha inasimamia masuala mazima ya ulinzi na usalama ukiachilia mbali masuala ya kiuchumi. Nimeshawahi kubahatika kuwa Kiongozi wa Dola katika mbili ya Wilaya katika Taifa hili. Nataka niwaambie tunaweza tukazungumza mambo hapa kwa sababu ya kishabiki na mihemko ya kisiasa, bila kuangalia masuala mazima ya hatma ya nchi. Ninachotaka kukisema, duniani kote ili watu waweze kukaa kwa amani na utulivu, ni lazima Serikali ijulikane kwamba ipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na suala zima la Serikali katika kuwekeza kwa Jeshi la Polisi. Yamezungumzwa maneno mengi, lakini nataka nikwambie sisi wenyewe Wabunge wa CCM haturidhishwi na hali ya Askari wetu wanavyoishi. Tunaiomba Serikali yetu ifanye hatua za makusudi, kwanza kuwapatia posho katika mazingira magumu ya kazi wanayofanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, utakumbuka, kuna wakati mimi kama Mkuu wa Wilaya ya Iringa, nimeletewa taarifa mabasi yametekwa pale Igunga.
MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumza na Askari, OCD hana mafuta ya kupeleka Askari. Haya lazima tuyaseme kwa sababu tusipoyasema tutakuwa hatulitendei haki Taifa letu. Natoa wito kwa Serikali yangu, natoa wito kwa Jeshi la Polisi, tengenezeni unit maalum itakayokuwa ina-deal na suala la kuhakikisha supply ya mafuta kwa Ma-OCD nchi nzima. Mafuta haya yasipite kwa Ma-RPC yaende kwa Ma-OCD kule kwa sababu wakati mwingine OCD anaweza akashindwa kumwambia bosi wake, tunao uzoefu huo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, Sekta ya Madawa ya Kulevya. Wiki tatu zilizopita kabla Bunge halijaanza, Kamati yetu tumefanikiwa kwenda kuangalia depot inayohifadhi madawa ya kulevya. Tumekwenda pale, mazingira wanayofanya kazi Askari wetu, Mheshimiwa IGP uko hapa, najua utanisikiliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba Jeshi la Polisi angalieni namna ya kuwasaidia Askari wanaopambana na watu wanao-deal na drugs muwa-treat kwa special treatment. Tumekwenda kumkuta binti mmoja anafanya kazi kwenye lile ghala ndani hana gloves, hana chochote, amevaa malapa ndani ya ghala la kuhifadhi madawa; ukiangalia ukuta umechakaa mpaka umeweka rangi ya njano. Sasa je, kwa binti wa Kitanzania anayefanya kazi; naliomba Jeshi la Polisi liweze kuwasaidia katika hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, tumekuwa tukizungumza suala zima la kupambana na madawa ya kulevya, lakini leo tunazungumza kwamba Jeshi letu la Polisi hawana hata boti za doria baharini. Linapotokea suala la kufanya surveillance kwenye bahari, hawana boti. Wanawezaje wakafanya kazi watu hawa? Natoa wito kwa Jeshi letu la Polisi na Serikali, naiomba Serikali ifanye kila inaloweza, wapatieni Polisi boti za kisasa, angalau tatu wakafanye doria baharini kupambana na masula mazima ya dawa za kulevya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho. Kuna mengi yamezungumzwa hapa, mambo ambayo kimsingi nimeshangaa sana! Namheshimu sana dada yangu Mheshimiwa Esther Matiko, ni rafiki yangu, nampenda, lakini kusema kwamba hotuba ya upinzani imezuiliwa, nimeshangaa kidogo. Kama mmezuia hotuba ya upinzani, hili naomba mlitolee ufafanuzi, kama kuna hotuba imezuiwa kusomwa hapa. Kwa sababu sijaona kama kuna hotuba imezuiwa kusomwa hapa Bungeni, unless otherwise kama kutakuwa kuna jambo lingine.
MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nimtie moyo kaka yangu Mheshimiwa Kitwanga, tumekwenda kwenye unit inayo-deal na kuangalia sample za madawa, ndani ya kipindi cha miezi mitatu, Mheshimiwa Kitwanga amesimamia, tumeona sample 256 za madawa ya kulevya ndani ya miezi mitatu. Leo tunavyozungumza mipaka yote hakuna madawa yanaingia kwenye nchi yetu. Mheshimiwa Kitwanga fanya kazi, tunakuunga mkono na sisi tunajua mnachokifanya kwa maslahi ya Taifa hili. Ahsante.