Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Baada ya kumaliza uchaguzi wetu wa nchi mwaka 2015, mlishangilia kwa mbwembwe nyingi sana kwamba Serikali na Chama cha Mapinduzi mmeshinda kwa kishindo, mkawaaminisha Watanzania kwamba mnaweza kuongoza nchi hii. Watanzania wakawasikiliza, mkaunda Serikali yenu. Tukaja Bungeni hapa tukaapishwa. Siasa za nje tukazileta Bungeni na ndiyo maana hivi vipaza sauti vimewekwa hapa kwa ajili kuzungumza. It is about talking! Ni juu ya dialogue hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali mnakuja na hoja zenu mnaendelea kuwashawishi wananchi kwamba sisi tuna uwezo wa kuongoza nchi hii, mnaleta hoja. Nasi tuliowapinga tunakuja na hoja zetu kuwakatalia kwamba hizi hoja haziwezekani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa leo hii Serikali inayosema ni ya Hapa Kazi Tu, Wabunge 250 wa Chama cha Mapinduzi na Serikali yao inashindwa kujibu hotuba ya kurasa 34! Inataka kuwaambia nini Watanzania? Kama kurasa ya 34 Wabunge 250 wa Chama cha Mapinduzi wanaogopa isisomwe, ninyi ni mature wa kuongoza nchi hii? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yetu tunakuja hapa tuna-dialogue, sisi ndivyo tunavyoiona Serikali, tunaoliona Jeshi la Polisi linafanyaje? Mikataba ya hovyo ikoje? Mtazamo wetu wa pili kwenye view yetu, this is how we see. Njooni na hoja mwoneshe udhaifu wetu uko wapi? Muwaaminishe Watanzania kwamba we are not matured. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kabla hatujaendelea, hatujazungumza, mnaweka mpira kwapani, mnataka msaidiwe na marefa. Suala la kujiuliza, you guys are you fit to lead this country? Kama hotuba ya ukurasa 30 hamwezi kuijibu, nani asiyejua mizengwe ya nyumba zilizouzwa katika nchi hii? Nani asiyejua nchi hii ina mikataba mibovu?
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Ambaye anatakiwa ashangiliwe kama King Kanuti, hatakiwi kuguswa katika Bunge hili. Nirudie maneno aliyozungumza Mheshimiwa Sugu; huyu Rais Mwema mnamfanya wananchi wasimwelewe. Yeye siyo Mungu, ana hali ya ubinadamu anaweza akakosea. Lengo letu hapa tupo kuisaidia Serikali na ndiyo dhana nzima ya kuwa na mfumo wa vyama vingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wamezungumza wenzangu hapa jinsi ambavyo mnawatumia Polisi, wakati wa uchaguzi mnawapa majina mazuri yote, lakini maisha wanayoishi ni ya shida sana. You are just using them! Mnawatumia wakati wa uchaguzi. Nawaomba ndugu zangu na niseme nyie mnaosema usalama wa nchi hii ni sababu ya ulinzi na usalama wa Jeshi la Polisi.
Mimi kama Mkristo na Mchungaji, Biblia inasema, Mungu asipoulinda mji, wakeshao wafanyakazi bure.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba utunze muda wangu tafadhali. Narudia tena, Bwana asipoulinda mji, wakeshao wafanya kazi bure! Biblia inasema mji haulindwi kwa wingi wa silaha anazokuwanazo mfalme. Ni Mungu ameamua ku-sustain amani ya nchi hii. Kama tutaendelea kucheza kwa kuamini kwamba bunduki na vifaru vitalinda amani ya nchi hii, tunapoteza muda. Ulinzi wa Muammari Gaddafi ulikuwa ni mkubwa kwa mbali kabisa kulinganisha na ulinzi wa nchi hii; lakini yuko wapi leo? Bwana asipoulinda mji, wakeshao wafanya kazi bure? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba Jeshi la Polisi, msitumike vibaya kisiasa, nchi hii ni ya mfumo wa vyama vyingi, sisi hapa hatujaja kwa fedha, tumekuja hapa kwa merit. Tuna haki hizo! Mnabambika watu kesi! Kama Mbunge, mimi nimebambikwa kesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siku ya uchaguzi, kulikuwa kuna yule Mungi sasa mmempandisha cheo ameenda bandarini. Ameagiza Polisi wanakuja kunivamia, wamepiga watu, wamevunja miguu, mikono, mwisho wa siku, wiki mbili zimepita sipelekwi Mahakamani mpaka nikaanza kudai na Wakili wangu kwamba mmetupiga, wakatulaza kwenye bwalo wanawake na wanaume! Mimi ninayezungumza! Tunadai kwa nini hamtupeleki Mahakamani? Napelekewa charge eti wewe umemjeruhi Kamanda wa Field Force. (Makofi)
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mimi Msigwa namjeruhi Kamanda wa Fied Force; na la pili nimejeruhi gari la Polisi. Kesi imekwenda Mahakamani wiki mbili, imefutwa; haina mkia wala miguu. (Kelele/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba Jeshi la Polisi, hebu acheni kutumika kisiasa. Tupo kwenye nchi ya vyama vingi. Kazi yetu kubwa hapa ni kuiweka Serikali sawasawa mwone wenyewe, nanyi Makamanda wa Polisi mnaona jinsi gani Serikali inashindwa kujitetea hapa! Kurasa 34 wanashindwa kujibu, they cannot! Nchi imejaa hofu, watu mmejaa hofu, huyu Rais mwema sana amewatia hofu mnaogopa kujitetea na kusema. Why? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Plato anasema: “if you cannot die for something, you are not worth living.” Sisi tupo tayari kwa lolote kwa sababu tunataka tuinyooshe nchi kwa faida ya vizazi vijavyo; na wajibu wetu ni kuikosoa Serikali, kuiweka vizuri. Haya tunayoyashauri, mangapi tuliwashauri? Tuliwashauri jambo la Katiba, mkalichukua, ila kwa sababu hamna ubongo wa kuku, mkashindwa. Si mlishindwa! Tuliwashauri, mkachukua. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliwashauri suala la elimu bure, mmejikanyagakanyaga, mnashindwa na yenyewe. Mngetupa hapa, hiki ni kisima cha kupata hekima na busara tunataka tuwashauri. You are incapable of leading this nation. Hapa ni mahali pa ku-dialogue. Ambao hamjasoma historia, nendeni Ugiriki mkaangalie Wagiriki walikuwa wanafanyaje kule Heathen. Unakuja na hoja unazijenga! Tumehamisha siasa kule, hapa ndiyo tunajadiliana, njooni na hoja. Sasa mmetunua macho, hamwezi kujitetea, mnajaza hofu watu, wafanyakazi na watu wote wana hofu, tutaendeshaje nchi hii? Bunge mmelifunga, halisikikii, humu ndani mnataka kutu-paralyse, sasa hiyo siasa tutafanyaje?
MHE. PETER S. MSINGWA: Ila saa hizi ni watu ambao hawaaminiki hata huko msiwaamini, hawaaminiki, saa hizi wanajikosha kusema sema maneno mazuri hapa wanawadanganya, tulikuwa nao usiku, waongo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, muda ukifika muafaka tutawataja, walikuwa wanatuletea na hela za kampeni sasa leo hapa wanajifanya wanadanganya danganya wanatuzunguka waongo, ni wanafiki hawa, hawawafai hata ninyi na hawa hawaifai hata Serikali kuwepo kwa sababu wata… (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Msigwa.