Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami nichagie hoja ya hotuba ya Waziri Mkuu ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2023/2024 na namshukuru Mungu kwa zawadi ya uzima na afya njema.

Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea maendeleo Watanzania, miaka miwili ya uongozi wake tumeshuhudia ubora wa miundombinu madarasa na vituo vya afya.

Mheshimiwa Spika, napongeza kazi nzuri inayofanywa na Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango. Pia nampongeza Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa kwa umahiri wa kazi kubwa anayofanya kumsaidia Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, mkoa wa Lindi haujaunganishwa na mkoa wa Mtwara au mkoa wowote kwa barabara kwa kiwango cha Lami. Tunaomba barabara inayotoka Masasi kupitia Nachingwea hadi Liwale ijengwe kwa kiwango cha lami mwaka huu 2023/2024, tafadhali tafadhali tumeahidiwa mara kadhaa haifanyiki.

Mheshimiwa Spika, tunaomba pia kupata maji safi na salama katika Kata za Ngunichile, Lionja, Mbondo kule Wilaya Nachingwea, hali mbaya bado akinamama wanahangaika kutafuta maji, wanakesha kutafuta maji hii ni hatari kwa usalama.

Mheshimiwa Spika, tunaomba ujenzi wa viwanja vya ndege Nachingwea na Lindi vijengwe kwa kiwango cha lami. Hii ni kwa sababu ya usalama, pia kinatumika na Mheshimiwa Waziri Mkuu anapoenda jimboni kwake Ruangwa, lakini pia kuna machimbo ya madini pale Nachingwea na Ruangwa, hii itavutia wawekezaji ndani na nje ya kupata usafiri wa uhakika, lakini pia Nachingwea kuna vikosi vya majeshi ya Jeshi la Wananchi Tanzania pia ni kwa sababu za kiusalama na utendaji kazi wao.

Mheshimiwa Spika, lakini pia Lindi kuna mradi mkubwa wa LNG hivyo kuhitaji usafiri wa ndege kwa saa 24 na wenye kiwango cha lami kwa mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja.