Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kupongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuwasilisha vizuri hotuba yake nzuri na utendaji wake mzuri sana, ameonesha weledi mkubwa sana katika uongozi wake. Pia nawapongeza Mawaziri wote waliopo kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kazi kubwa wanazozifanya kuhakikisha nchi yetu inapiga hatua kimaendeleo. Nawapongeza pia Makatibu Wakuu wote kwa utendaji uliotukuka.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita katika suala zima la ajira kwa vijana. Nchi yetu kumekuwa na tatizo kubwa la ajira kwa vijana wetu, lakini pia kuna vijana ambao wapo katika ajira zisizokidhi haja na mfano vijana wanaofanya vibarua TPA, wanafanya vibarua kwa miaka 10 lakini ajira zinapotokea wanaletwa wengine na wale wanaofanya kazi ya kibarua wanaendelea kuwa vibarua. Mfumo wa kutumia wakala wa vibarua kama vile SUMA JKT unadumaza maendeleo ya upatikanaji wa ajira kwa sababu wanatoa ajira za kutwa na hakuna njia nyingine.

Naiomba sana Serikali iangalie upya utaratibu wa utoaji ajira kwani kuna vijana wengi wanajitolea bure kutoa huduma kwa zaidi ya miaka mitano, lakini ajira zinapotokea hawapewi kipaumbele. Hali hiyo sio nzuri inakatisha tamaa sana kwa vijana wetu. Vijana wanaojitolea wapewe kipaumbele. Niipongeze Serikali kwa kuja na utaratibu wa intern kwa vijana, ni jambo jema, lakini vijana wengi wako intern lakini tuhakikishe kuwa hao walio intern wanapata ajira za kudumu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.