Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN: Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia afya njema na uzima.

Pili, natoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuliongoza vizuri sana Taifa letu. Aidha, nakupongeza wewe Mheshimiwa Spika, Naibu Spika na wasaidizi wako wote kwa kuendesha vikao vya Bunge kwa umakini na umahiri kabisa.

Mheshimiwa Spika, lakini pia naomba kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa wasilisho zuri na hotuba yenye kuleta matumaini kwa ustawi mzuri wa Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizo, naomba kuchangia sehemu mbili tu nazo ni ushirikiano kwa Taasisi za SMZ na Taasisi za SMT.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Waziri Mkuu ni kiungo muhimu sana katika kutatua changamoto mbalimbali za Tanzania Bara na Zanzibar kupitia Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar. Nazipongeza ofisi hizi kwa kazi nzuri wanazozifanya, lakini bado kuna haja kuendeleza ushirikiano kwa taasisi za zetu ambazo sio za Muungano Kikatiba. Mfano Afya, Maji, Uwekezaji, Utalii na kadhalika, kwani ushirikiano huo kasi yake ikiongezeka basi itakuwa na mafanikio kwa SMZ na SMT na Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, pili ni masuala ya mazima ya kupambana na masuala ya udhalilishaji na ukiukwaji wa maadili. Matendo ya kujamiiana ya jinsia moja au ndoa za jinsia moja sambamba na uharibifu wa vizazi vyetu kwa maana watoto wetu. Jambo hili ni hatarishi sana kwa ustawi mzuri wa Taifa letu. Hivyo naiomba Serikali na Watanzania kwa ujumla kukemea na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria zetu na Katiba yetu.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa naunga mkono hotuba hii kwa asilimia mia, ahsante sana.