Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nikushukuru, lakini pia nimshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kunijalia afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu katika Wizara ya TAMISEMI utajikita sana katika mambo matano. Mambo ambayo nitajitahidi kuchangia kama muda utanifaa au ntapata muda wa kutosha nitachangia kuzungumzia ufinyu wa nguvu kazi, nitachangia kuhusiana na mifumo ya kazi, nitachangia pia kuhusiana na changamoto ya kimaadili, nitachangia pia kuhusiana na tatizo la ajira na jinsi ya kulitatua lakini pia nitazungumzia ushauri jinsi gani tunaweza tukatatua baadhi ya changamoto kama muda utanitosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kusema kwamba Wizara ya TAMISEMI ni Wizara kubwa lakini ni Wizara muhimu sana na Wizara hii ni mtambuka. Pamoja na umuhimu wake na ukubwa wa Wizara hii kama Wizara nyingine kwenye nchi hii zina changamoto. Changamoto kubwa iliyoko katika Wizara ya TAMISEMI iko katika ufinyu wa nguvukazi. Licha ya kwamba kuna changamoto nyingine lakini eneo hili naliona ni eneo ambalo lina sumbua sana kiasi cha kufanya kwamba hata utekelezaji wake wa majukumu ukawa hauwezi kwenda sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, shida iliyoko hapa kuna uchache wa watendaji lakini hata wale walioko baadhi yao ni wachache tu ambao ni bora kwa maana ya kwamba quality. Hata hao wenye quality bado baadhi yao wanakosa weledi. Hali hii inasababisha changamoto nyingi zikiwapo ni pamoja na hasara zinazojitokeza katika maeneo mbalimbali hususani katika maeneo ya walaji kwa maana ya halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi mingi inayokwenda kule kutokana na changamoto nilizozigusia hapo zinasababisha kusimamiwa na watendaji ambao baadhi yao hawana weledi lakini wengine hawana sifa lakini hata ufahamu wa jinsi ya kufanya hiyo kazi aliyotumwa inakuwa shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na u-sensitivity wa taarifa ambazo nitazitoa sitataka kuzungumza in details hizi taarifa. Nitazungumza tu generally. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kuna watu wamepewa kazi ilikuwa ni ya injinia lakini amepewa mtu wa certificate na hana uelewa wa kufanya kazi hiyo, hali ambayo imepelekea kutokea na hasara kubwa katika usimamizi wa miradi hususan katika miradi ya elimu pamoja na miradi ya afya. Kama nilivyosema sitataka kwenda kuingia kwenye details ninazungumza tu generally ninafikiri hizi details nitazituma kupitia mchango wa maandishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto ya mifumo pia, mfumo unaotumika hapa TAMISEMI, mifumo ya kifedha kwa mfano haioani, hashirikiani, haisomani. Unaweza ukakuta kuna taarifa zinatakiwa zipelekwe zinakwenda taarifa ambazo si sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika kumekuwa na changamoto ya watendaji kukaidi taratibu za utekelezaji wa majukumu yao, pia kukaidi maelekezo kutoka kwenye mamlaka zinazowatuma. Pia, kama nilivyosema, kwamba nahitaji kuzungumzia kidogo kwenye tatizo la ajira. Hapa naomba kidogo kama ushauri. Kwa bahati nzuri tulikuwa na ajira mwaka jana au muhula uliopita, zile ajira kwa kweli zimetuletea changamoto kubwa sana Wabunge, zimetuletea changamoo kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu gani? maeneo yote takribani ya vijijini kuna shida ya ajira; na ajira zimetangazwa na wengi wamekuwa na matumaini kwamba kwa namna moja au nyingine wanaweza wakazipata lakini kilichotokea ni kwamba kuna maeneo hawakupelekewa kabisa; yaani kwamba watu hawakuajiriwa lakini kuna maeneo mengine wameajiriwa idadi ya watu wengi. Hatutaki kuzungumza kwamba wapi ilikuwa vipi lakini kwa mfano tu mimi Jimboni kwangu katika ajira zote zilizotoka za elimu pamoja na shule ni watu wawili tu ndio walipata ajira ile, kwa kweli sio fair ilhali kuna idadi ya watu wengi sana ambao wamekosa ajira na lakini wamesoma na wanatarajia pia na wanaomba. Kwa hiyo unapopeleka watu wawili katika jimbo zima sidhani kama huu mgawanyo wa cake uko sawa, naliomba jambo hili tuliangalie kwa umakini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashauri kwamba katika hizi ajira 21,000 basi tutenge ajira 5,000 zibaki kwenye wizara kama msawazo lakini zile ajira nyingine yaani kwamba 21,000 ukitoa 5000 hizo zitakazobaki tuzigawe kimajimbo. Tuangalie proportional amount ambayo kila jimbo inaweza ikapata, kila jimbo lipate kwa kiwango kadhaa, halafu zile zingine 5,000 ndizo ziende katika kufuata hizo taratibu ambazo mlizfanya huko nyuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naomba kuunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)