Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ALI HASSAN OMAR KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii. Kwanza nimpongeze mzungumzaji aliyemaliza kwa shairi lake kilichochema ni chema hakibadili tabia. Tabia ya Maalim Seif ni kushindwa uchaguzi na nashangaa kwa nini mnamwachia aendelee na tabia hiyo hiyo na ataendelea kushindwa tu. Kwa hiyo, kwa kuwa hakibadili tabia siku zote atashindwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichangie katika nyumba zitakazojengwa kwa Jeshi la Polisi kwa Zanzibar. Tuweke proportion ambayo ni nzuri, lakini cha pili mawasiliano ya redio kwa Zanzibar askari wanaongoza kwa simu kule, kwa hiyo, hili nalo pia ni muhimu tulitazame. Kingine masuala ya umeme wanalipa Wakuu wa Vituo wakati mwingine, kwa hiyo na hili liangaliwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nizungumzie jambo moja, amesimama hapa kuna mtu alijiita mchungaji, lakini nikimnukuu ndugu yangu mmoja alisema sijui kanisa hilo hawa wafuasi watakuwa wakoje, mimi sisemi. Anasema kwamba, Wabunge 250 wanashindwa labda kuzijibu hoja, upinzani hauna hoja, hapa hawana hoja, hawana ajenda za kuzungumza sasa hivi wamekuwa ni virukia, kuna miti inaitwa virukia haina mizizi. Ikitajwa Lugumi wanajipaka damu za simba kama wao ndio waliomuua simba, ninyi sio, wako wenyewe waliofanya hiyo kazi, mnajipaka damu halafu mnajisingizia ninyi ndiyo mlioua simba, hamna hoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Toka wauvae ulitima kwa kulamba joka la ufisadi sasa wanadandiadandia, kwa hiyo hawana hoja ya msingi. Lakini Mheshimiwa Lwakatare kule amesema amethibitisha kwamba, wanatangwa maji kwenye kinu na hayabadiliki kwenye kinu hayawezi kupita smoothly kwa sababu ya kuyatwanga kwenu. Watu wanawashuhudia hata mngeletewa hiyo TV katika hoja zenu za kurukiarukia basi pia msingefanya kitu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa wale waliokuja na habari za matukio jamani mnasahau? Hamtajwi matokeo ya mabomu nyie? kuwamwagia watu acid, kuwaua ma-padre mbona hamtaji kama huu ni uvunjifu wa amani, mnazungumza hoja gani katika hili? Zungumzeni kitu ambacho kitaleta amani na utulivu katika nchi hii, wadau wa amani na utulivu wanajulikana na wanaochafua wanajulikana mahali popote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe unalalamika kupelekewa askari Zanzibar, unalalamika nini, wewe ndiyo mhalifu kama unalalamika, kwanini unakataa kupelekewa askari kama sio mhalifu. Sasa hili ni lazima liangaliwe, nikija kuchangia katika hoja nyingine amezungumzia Mheshimiwa Waziri katika utekelezaji wa bajeti iliyopita kwamba, wamejaribu kuzuia biashara haramu ya kuuzwa watu, hili jambo bado lipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna ndugu zetu wanapelekwa Oman, Dubai, wanapelekwa Bara Arab wanakwenda kutumikishwa bila ya hiari zao, mikataba inaondoka hapa mingine na wakifika kule wanafanyiwa mambo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuunga mkono hoja hii mimi labda hapa nizungumzie kitu kimoja, kuna wenzetu wanajaribu kulipaka matope jeshi letu la polisi, amani na utulivu wa nchi yetu ya Tanzania basi Jeshi la Polisi ndiyo mchango wake mkubwa na waharibifu wa amani hiyo na utulivu ndiyo hawa, nashangaa. Kuna msemo unasema homa mpe paka, maana yake homa mpe paka kwamba wewe kwa kuwa unaumwa ikutoke homa ile kwa kuwa paka haitomdhuru. Sasa hicho sio kitu sahihi wanachokifanya, tunapozungumzia amani na utulivu, majeshi yetu yanakwenda vizuri, kwa hiyo, tunashukuru kwa kutusaidia katika kuweka sawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia hapa jambo lingine ambalo ni muhimu sana, ni usafiri kwa Jeshi la Polisi kwa Mkoa wangu wa Mjini Magharibi Unguja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante sana.