Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia Wizara ya TAMISEMI. Kipekee nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa kutuletea fedha nyingi sana pamoja na miradi hasa katika Majimbo ambayo yalikuwa yamesahaulika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukubali ukweli Wabunge tunatoka kwenye Majimbo ambayo yana historia tofauti. Jimbo la Nkasi Kusini lilikuwa halina miundombinu, miundombinu imeanza kujengwa ndani ya kipindi cha Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu la Nkasi Kusini lilikuwa na Kituo cha Afya kimoja tu, nacho kilikuwa hakijakamilika kwa hiyo ina maana mimi nimeingia ndani ya Jimbo la Nkasi Kusini halina Kituo cha Afya na lina Kata 11 na umbali wa kutoka Kata moja kwenda Kata nyingine kuna umbali wa kilomoita 40 mpaka 50, kwa hiyo Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI naomba mgao wa Kata ili huduma za kijamii wananchi waweze kupata kwa uraisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo langu linapakana na Nchi za Jirani Ukanda wa Ziwa Tanganyika. Kule kuna makambi ya wavuvi ni maeneo mazuri sana kwa uchumi lakini wananchi wamekuwa wanaishi katika mazingira ambayo kuna uhalifu wa mara kwa mara, ndani ya miaka mitatu wamevamiwa mara sita. Vipo Vijiji karibia ishirini ambavyo viko mwambao wa Ziwa Tanganyika ambapo hali ya hewa ikichafuka, Ziwa likichafuka usafiri wao ni ndani ya Ziwa Tanganyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawana mbadala kwa hiyo wakinamama wajawazito wanapoteza maisha, wakinamama hawapati huduma ya afya na hata huduma za jamiii ambazo Mheshimiwa Rais anatoa kwa ajili ya maendeleo kufika kwake tu kule hakuna barabara, hakuna miundombinu. Mheshimiwa Rais ametoa magari ya kuchimba visima, tulikuwa tunajadili na Wakurugenzi wa Maji, namna ya vifaa vile kufika kule kuchimba visima hakuna kwa sababu hakuna barabara. Nikuombe Mheshimiwa Waziri tena nikushukuru sana hiyo timu mnaenda kwa kasi mmevaa kiatu cha Mheshimiwa Rais, nawapongezeni sana. Kwanza ni wasikivu, mlituita tukakaa tukawapa vipaumbele vyetu vya Majimbo na tumeishawapa tunaomba mtekeleze. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Nkasi Kusini lina Vijiji ambavyo havina maboma, vingine vina maboma wananchi wamejitolea kwa nguvu zao, maboma ya zahanati na maboma ya shule pia baadhi ya shule hazina madawati nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri, mje na mkakati maalumu kwa sababu ya kuleta madawati pamoja na viti shule za msingi kuna hali mbaya sana Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo shule ambazo watoto mpaka sasa hivi wanasoma chini ya mwembe (chini ya mti) na huo ni mfano wa Kijiji cha Tundu, Mkomachindo, Kapumpuli, Kilambo cha Mkolechi, Tuondokazi, Msamba, Lyela, Mwinza, Izinga, Katani, Kata, Yapinda, Isambara, King’ombe kuna Vijiji ishirini wanafunzi wanasoma chini ya mti Pamoja, kijiji kimoja wanafunzi wanasoma chini ya mwembe, vijiji vingine wanakalia mawe! Karne ya Ishirini na moja wanafunzi wanakalia mawe hata elimu wanayoipata wanaipata katika mazira magumu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Rais ametangaza hizi ajira ninakuomba Mheshimiwa Waziri kwa sababu kuna mazingira ambayo ni magumu, tuleteeni fomu sisi Wabunge, tumepita huko kero na mazingira tunayajua tujaze fomu mazingira yale ambayo watumishi waende moja kwa moja. Kwa sababu mkiwapeleka kule wataishia Mjini wata robu kwa hiyo wanafunzi wa nchi hii hawatapata haki ya walimu wanao husika kwa sababu kuna shule nyingine kuna mwalimu mmoja nyingine hakuna wana azima kutoka shule jirani kwa hiyo ajira hizi tuleteeni fomu tuwape vipaumbele vya maeneo yetu yenye changamoto ili mnapo ajiri waende moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo ahadi za viongozi, ahadi za viongozi hizi wanapofika kwenye Kata zetu wananchi wana amini sana Viongozi Wakuu wa Nchi yetu. Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye kampeni alihaidi Ujenzi wa Kituo cha Afya Tarafa ya Chala ni Makao Makuu ya Tarafa ambapo Kata hii Kituo chake hiki kina hudumia Kata Tatu. Kina hudumia Kata ya Ntuchi, Kata ya Katumbila na Kata ya Chala, ambazo mpaka sasa hivi kuwa ahadi ya Mheshimiwa Rais lakini bado hakuna kinachoendelea, akaja Mheshimiwa Katibu Mkuu Kiongozi wa Chama Mheshimiwa Daniel Chongolo nae kahaidi Ujenzi wa Kituo cha Afya Chala nacho bado, akaja Mheshimiwa Waziri Mkuu kapita napo katoa maagizo kijengwe Kituo cha Afya Chala pia Hayati Mheshimiwa John Pombe Magufuli nae alitoa ahadi ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Chala bado mpaka sasa. Ahadi ya Viongozi Wakuu wa Nchi karibu watatu bado maandalizi Mheshimiwa Waziri, naomba Kituo cha Afya Chala kianze kujengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia zipo Kata ya Sintali, Miula wananchi wanapata huduma ya mbali sana wanatoka maeneo wanatembea karibu kilomita 20 mpaka 40. Naomba Kata ya Sintali, Kata ya Miula pamoja na Kata ya Chala ijengewe Vituo vya Afya. Ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)