Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru na nimshukuru Mungu kwa kupata nafasi hii mchana huu wa leo ili niweze kuchangia. Naishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa ambayo imeendelea kuifanya katika Halmashauri yetu ya Mji wa Bunda ambapo kwa kipindi hiki cha takribani miaka miwili na sehemu tumeshapata fedha za maendeleo kwenye idara ya elimu, afya na TARURA, zaidi ya shilingi biloni 10, tunaipongeza Serikali. Pamoja na kwamba bado kwenye maeneo hayo kwenye barabara za TARURA bado tuna changamoto, tuiombe Wizara iendelee kuwasaidia hao watu wa TARURA kwa kuwatengea fedha za kutosha ili miundombinu yetu ya barabara kwa wananchi yetu iweze kutekelezwa vizuri.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni kuhusu TACTIC. Halmashauri ya Mji wa Bunda tupo kwenye ile miji 45 inayoendelezwa. Wananchi wa Jimbo la Bunda Mjini mradi huu wanausubiri kwa hamu kubwa; na kwa sababu tulishawapa matumaini makubwa na kadri ambavyo viongozi wetu wamepita katika Wilaya yetu wakatoa ahadi kwenye mradi huu, ningeiomba sana Serikali ya Awamu ya Sita na Wizara ya TAMISEMI kuhakikisha kwamba mradi huu unatekelezwa kabal aya 2025. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mji wa Bunda tulipata katika mradi huu lami kilomita 25.3, soko jipya la kisasa, machinjio, stendi na dampo la uchafu. Sasa, vitu hivi visipotekelezwa kwa kipindi hiki vinaenda kuwakatisha wananchi wetu tamaa. Kwa sababu jiografia ya Mkoa wa Mara mtu yeyote anayetokea Mwanza Kwenda Mkoa wa Mara anapitia Bunda. Kwa hiyo jiografia ya Mji wa Bunda ikikaa vizuri inaleta jiografia nzima ya Mkoa wa Mara kaukaa vizuri. Kwa hiyo ni ombi langu kubwa kwa TAMISEMI kuwaomba kwamba mradi huu wa TACTIC uwewze kutekelezwa vizuri. Kwa sababu jambo hili…

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mhehsimiwa Robert Maboto, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Cosato David Chumi.

TAARIFA

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi naomba kumpa Mheshimiwa anayezungumza taarifa kwamba, kufanikiwa na kutekelezwa kwa haraka kwa mradi wa TACTIC katika miji 45 likiwemo Jiji la Mbeya, pamoja na kuboresha miundombinu itasaidia halmashauri hizo kuwa na miradi ambayo itakuwa chanzo cha mapato ambayo baadaye itaipunguzia Serikali mzigo kwa hiyo ni muhimu ikatekelezwa kwa wakati, naomba kuwasilisha.

SPIKA: Mheshimiwa Maboto, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, naipokea kwa sababu na yeye ni mhanga kama mimi hapa. Kwa hiyo jambo hili kwa wananchi wetu ni jambo muhimu sana na ni vizuri kwa Serikali kwa sababu ilishatoa ahadi kwa wananchi ikatekelezwa. Pia itasaidia kuifanya halmashauri iweze kupata vyanzo vya mapato. Kwa mfano, stendi yetu ya Bunda Mjini mabasi yote ya Mkoa wa Mara yanayokwenda Mwanza yanayotoka nje ya Mkoa wa Mara lazima yapite kwenye Halmashauri ya Mji wa Bunda. Kwa hiyo ni hakika kwamba mradi huu ukitekelezwa utawafanya Halmashauri yetu ya Mji wa Bunda na wananchi wote wa Bunda kwa ujumla kuona kwamba wamepata mapato ya kutosha katika Halmashauri yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni maombi maalumu kwa ajili ya jengo la Makao Makuu ya Utawala Halmashauri ya Mji Bunda. Jengo hili lilishajengwa, lakini tatizo la jengo hili halina uzio. Kwa hiyo kwa sababu jengo hili limejengwa na halina uzio kwa hiyo mtu anaweza akatokea mahali pengine popote kuingia katika Halmashauri ile. Kwa hiyo hata namna ya kufanya ulinzi kwenye eneo lile inakuwa ni ngumu. Ombi langu ni kuiomba Wizara iendeleee kutenga bajeti kwa ajili ya ukamilishwaji wa eneo hili. Bado tunahitaji uzio, tunahitaji mitaro ya uturirishaji maji na hakuna ghala la kutunzia vifaa. Ukiingia kwenye lango la Halmashauri kwenye jengo hilo pale kwenye mlango unapoingilia ndipo unakuta Halmashauri wamelaza nondo hapo na cement kwa ajili ya maendelezo mengine ya shughuli za maendeleo katika Halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Spika, ombi lingine ni kuhusu maboma ambayo yalijengwa na wananchi katika Halmashauri yetu ya Mji wa Bunda ambayo bado haijakamilishwa. Wananchi walijitolea nguvu zao, wakafanya kazi kubwa na sasa wanaomba ukamilishwaji.

Mheshimwia Spika, kuna Shule ya Msingi Bigwitu yako majengo mawili, Shule ya Msingi Bikole lipo jengo moja, Shule ya Msingi Kabarimu yako majengo mawili na Shule ya Sekondari Mpya ya Kata ya Nyamakokoto mbayo Serikali imeweka pale fedha zaidi ya milioni 500, lakini kulikuwa pia kuna na nguvu za wananchi pale ambazo wao walikuwa wameshajenga majengo yao pale. Ukamilishwaji wake; tuiombe TAMISEMI sasa itusaidie kuhakikisha kwamba jambo hili linakamilishwa ili Halmashauri ya Mji wa Bunda uweze kukaaa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho ni kuiomba Serikali. Suala la ajira hizi ambazo zimetolewa na Serikali, nimalizie, kwa kumalizia tu; iligawanywa katika mikoa yote. Hapa tulipo simu za wananchi ambazo tunazipata kwa ajili ya kutuambia tuwafanyie mpango ili wapate ajira Serikalini ni simu ambazo hatuna majibu. Ukitengenezwa mgawanyiko wa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na naunga mkono hoja.