Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. ALEXANDER P. MNYETI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Nianze kwa kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika Taifa letu, hususan katika Jimbo letu la Misungwi, kwa sababu mambo mengi tumeyaona Mheshimiwa Rais ameyafanya katika sekta za afya, elimu na maeneo mengine. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya.

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza ambalo nataka niishauri TAMISEMI. Mheshimiwa Waziri anafanya kazi nzuri sana na wasaidizi wake. Kwa bahati nzuri anafahamu kwamba mimi nimefanya kazi Serikalini, kwa hiyo Mawaziri wajanjawajanja wote nawajua na wasanii wote nawajua kwa sababu tumefanya kazi kwa pamoja kwa muda mrefu, lakini nataka niseme kwamba Mheshimiwa Angellah Kairuki ni Waziri imara sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, iko changamoto kubwa ambayo Waheshimiwa Wabunge wamejaribu kuieleza sana. Hii kero kusema kweli hata jimboni kwako najua ipo, yako maboma ambayo wananchi wetu wameyajenga wakafikia kwenye maeneo ya lenta na wengine wakamaliza maboma. Maboma hayo yametelekezwa miaka kumi, mengine miaka 15, lakini Serikali kupitia nyaraka mbalimbali ilizokuwa ikizitoa kule vijijini ilikuwa inahamasisha wananchi wajenge yale maboma, wakishamaliza Serikali imalizie. Hata hivyo, Serikali haijamalizia hayo maboma. Tunaomba sana kwa Mheshimiwa Waziri, ziko zahanati wananchi wamejenga, yako madarasa wananchi wamejenga, wanaomba yakamilishwe.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, ziko halmashauri nyingi sana ambazo hazipeleki asilimia 40 vijijini. Pesa zote zinaishia pale halmashauri wanatumia wanavyotaka asilimia yote 100 na haiendi kule vijijini. Tunaomba sana Mheshimiwa Waziri alione hili na alifuatilie kwa karibu sana kwa sababu yamekuwa ni malalamiko ya Wabunge wengi na wanahitaji kujua asilimia 40 zina matumizi gani kule vijijini.

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu, kule Misungwi naishukuru sana Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mama Samia na usimamizi wa TAMISEMI nilijengewa hospitali ya wilaya, nashukuru sana, zaidi ya majengo kumi yameshakamilika, lakini majengo haya hayana vifaatiba. Mheshimiwa Waziri akiacha kuyapelekea vifaatiba na mwaka huu maana yake yatabaki kuwa white elephant kwa mwaka mzima hayafanyi kazi na mwisho wa siku yataanza kuchakaa.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho, namwomba sana Waziri amthibitishe Mkurugenzi wangu awe Mkurugenzi rasmi. Tumekaa naye miaka mitatu amefanya kazi nzuri. Mapato tuliyokuwa nayo toka bilioni mbili kwa mwaka sasa tuna bilioni nne, lakini mwisho wa siku watu wazuri kama hawa huwa hawataki kuwathibitisha, wanawahamisha wanawapeleka maeneo ya wajanja, sisi tunabaki tunatoa macho. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri huyu Mkurugenzi ametufanyia kazi ya heshima Wanamisungwi, tunamhitaji, tunaomba wamthibitishe ili aweze kufanya kazi yake vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)