Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, location ya Jimbo la Manispaa ya Iringa, lipo katikati ya majimbo mengine ya Mkoa wa Iringa, hivyo kusababisha watu kutoka katika Mkoa wote wa Iringa kuona urahisi wa kufuata huduma za muhimu ndani ya Manispaa ya Iringa. Hii imesababisha uhitaji wa huduma za jamii kama afya, elimu, miundombinu ya barabara kuwa changamoto, kwani tunalazimika kuhudumia watu wengi zaidi ya wakazi waliopo ndani ya mji. Mfano Hospitali za Wilaya za Jimbo la Kilolo imejengwa Wilayani Kilolo ili watu wafuate huduma hiyo Kilolo wanatakiwa kupita Manispaa ya Iringa.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa hali ya kawaida hawezi kupita mjini kwenda kuifata hospitali iliyoko Kilolo. Wanatakiwa kutibiwa Manispaa, jiografia hiyo iko pia kwa Jimbo la Isimani na Kalenga.

Hivyo tuna umuhimu wa kuongeza vituo vya afya pembezoni mwa Jimbo la Iringa, ambayo ni Kata ya Kitwiru, Kata ya Igumbiro na Kata ya Isakalilo. Pia utanuzi wa Hospitali ya Frelimo uende kwa kasi na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa ili kuhimili uhitaji uliopo.

Pia shule kongwe kama Iringa Girls, Lugalo Sekondari na Mawele Wele Sekondari, ziongezewe mabweni kwa kuwa ni shule za kitaifa halafu zinachukua watoto wenye ulemavu wa kila aina. Sasa zinazidiwa sana wakati zina maeneo ya kutosha kufanya expansion. Iringa Girls imaliziwe yale mabweni mawili ambayo hayakumaliziwa wakati wa ukarabati wa shule kongwe ambayo ni bweni la Mshikamano A na B.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa madarasa kwenye maeneo yetu uzingatie uhitaji, kuna sehemu nyingine shida kubwa inakuwa sio tu madarasa bali majengo mengine. Pia fedha za ujenzi wa mabwalo ziangaliwe upya na zitolewe sawa kati ya TAMISEMI na Wizara ya Elimu, wengine wanatoa chache wengine nyingi, baadhi mabwalo yanaisha kwingine inashindikana. Ndani ya Manispaa tunaomba mabwalo yamaliziwe katika sekondari zetu ambayo hayajakamilika. Kama Kwakilosa Sekondri, Mlandege Sekondari, Tagamende Sekondari na kadhalika.

Pili, Iringa Manispaa imekuwa na shida kubwa ya mara kwa mara vifungu ku-burst hivyo kusababisha uendeshaji wa halmashauri kuwa mgumu na kuwakosesha Madiwani kulipwa posho za vikao kwa wakati na kuwalipa wazabuni wa Manispaa na kuendesha shughuli nyingine, hili lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Spika, pia ulipaji wa madeni makubwa kama deni la Kampuni ya SIETCO, wanaoidai Manispaa pesa za ujenzi wa stendi ya Igumbiro na soko la Mlandege vilipwe ili kuondoa hasara ya kulipa penalt na kuja kuzuia wahisani kutoa misaada pia.

Mheshimiwa Spika, TARURA tunaomba sana kwa namna Mji wa Iringa ulivyokaa, unapitiwa na barabara kubwa za kimataifa mbili (TANZAM). Iringa Manispaa inapitiwa na barabara kubwa ya kutoka mikoa kumi ya Kusini kwenda Mashariki ya nchi yaani Mbeya – Dar es salam; pia inapitiwa katikati na barabara inayotoka Cape Town to Cairo yaani mikoa 10 ya Kusini mwa Tanzania ikiwemo Nyanda za Juu Kusini kwenda mikoa sita ya Kanda ya Ziwa na Kaskazini mwa nchi mikoa sita. Sasa jaribu kufikiria huo mzigo unaopita Iringa wakiwemo na wakazi kutumia barabara hizo hizo. Ni shida kubwa sana na kumekuwa kuna mkwamo na ajali nyingi sana.

Mheshimiwa Spika, tunaomba barabara za ndani za Mji na Manispaa ya Iringa zijengwe kwa kiwango cha lami ili kuufungua mji ule ili angalau wanancchi watumia barabara za pembezoni ili kupisha watumiaji wa Kimataifa watumie hizo nyingine. Mfano barabara ya Ipogolo – Kagrieolo - Kitwiru; Wilolesi - Mtwivila; Magereza - Ipogolo; Don Bosco - Kihesa Kilolo kupitia Magic Site, pia kukamilishwa kwa Iringa bypass.

Mheshimiwa Spika, otherwise tunawashukuru sana kwa juhudi kubwa na kazi inayotukuka inayofanywa na TAMISEMI kwa ujumla.