Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, kwanza Halmashauri nyingi zinakosa ma-engineeer wa kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa hali inayosababisha miradi mingi kutekelezwa chini ya kiwango. Mfano katika Halmashauri ya Newala ina maafisa mchundo wanne, engineer mmoja na hakuna mkadiriaji majengo. Athari ya hali hii ni kwamba miradi inayotekelezwa kwa force account mara nyingi inaponunua vifaa kwa jumla (bulk procurement) ukadiriaji unakuwa na mapungufu mfano wengi hununua vifaa vingi vinavyobakia hali inayoleta ubadhirifu wa fedha za umma.

Pili ni kuhusu miundombinu chakavu nikianza na afya; vituo vya afya vya Chihangu na Mkwedu; tuna vituo vya afya viwili ambavyo ni kongwe na chakavu; havina wodi za kulaza wagonjwa.

Kuhusu uchakavu; Kituo cha Afya Chihangu paa lake linavuja sana hali inayoleta ugumu kwenye utendaji kazi kwa watumishi na wagonjwa pia.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa elimu; shule nyingi za msingi ni za muda mrefu na zimechakaa sana. Mfano ni shule zifuatazo; Nakahako (paa linavuja) namadarasa matatu ni mabovu inabidi yavunjwe hayakarabatiki; Shule ya Msingi Mtanda; Mtongwele; Nambudi; Mpotola; na Bahati (vyumba vichache). Pia Majembe Juu; Chinle; Lihanga na Mahoha.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Newala ina upungufu mkubwa wa nyumba za watumishi.