Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na mama yetu, Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Wilaya ya Muleba mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia Wizara ilitenga shilingi 500,000,000 kuanza ujenzi huo. Ujenzi ulianza kwa majengo mawili ya OPD na maabara. Nimesoma bajeti nzima ya Wizara kwa mwaka 2023/2024 hakuna sehemu ambayo Serikali kupitia Wizara imetenga fedha kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muleba. Wilaya ya Muleba ni moja ya Wilaya kongwe hapa nchini ambayo ilianzishwa mwaka 1974 lakini hadi leo haina Hospitali ya Wilaya. Namshukuru Rais wetu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha shilingi 500,000,000 kuanzisha ujenzi wa hospitali hii.

Mheshimiwa Spika, kwa heshima na taadhima, angalia popote, naomba fedha angalau shilingi 500,000,000 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muleba kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Nakushukuru sana kwa kunipatia hiyo fedha.

Mheshimiwa Spika, pamoja na maombi ya Hospitali ya Wilaya, naomba fedha kwa ajili ya Kituo cha Afya Kata ya Kimwani. Ni kata yenye watu wengi sana lakini pia inahudumia kata mbili za visiwani za Mazinga na Ikuza.

Mheshimiwa Spika, nina barabara tatu muhimu lakini kutokana na jiografia yake zinahitaji nguvu zaidi nje ya bajeti ya TARURA Wilaya. Baraza hizo Kimeya - Burigi (Kata za Kasharunga na Karambi), Ruhunga -Kiholele (Kata za Magata Karutanga na Bureza), Kasenyi-Rwazi (Kata Ikuza).

Mheshimiwa Spika, pamoja na timu nzima ya Waziri nina imani kubwa na ninyi. Natumaini maombi yangu yatapata kibali machoni pako.