Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, nianze kuhusu ukubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga/Jimbo la Mbinga Vijijini; Halmashauri hii ni kubwa, ina kata 29, naomba kuleta maombi ya kuigawa, jambo ambalo tayari vikao vya ushauri Wilaya na Baraza vimeridhia. Kugawanya kwa Halmashauri hii kutasogeza huduma karibu na wananchi tofauti na ilivyo sasa wananchi wanafuata huduma hii mbali kiasi cha kutumia gharama kubwa za usafiri na kutumia muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, maombi ya mgawanyo wa Halmashauri yaende sambamba na mgawanyo wa Kata za Litembo, Litumbandyosi, Langiro, Maguu, Linda, Nyoni, Matiri, Ngima, Mkumbi na Maguu. Kata hizi ni kubwa kimaeneo lakini pia na idadi kubwa ya wakazi kiasi cha kuleta ugumu kwa watumishi na watoa huduma zingine kuwafikia wananchi kwa wakati. Ikiwa hoja hizi zitakuwa na ugumu katika utekelezaji wake niombe huruma ya Serikali ya kuongeza fedha kwa ajili ya Mfuko wa Jimbo na mafuta ya kuwezesha kuwafikia wananchi kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, kuhusu maombi ya vituo vya afya vya kimkakati; naleta ombi la vituo vya afya vya kimkakati kutokana na maeneo haya kufuata huduma hiyo mbali au nje ya wilaya yaani Wilaya ya Nyasa. Hivyo naomba Kituo cha Afya Mbuji, Tarafa ya Mbuji ambayo inakata za Mpapa, Nyoni, Mbuji, Litembo na Kitura haina kituo cha afya hata kimoja, pamoja na Kituo cha Afya Ukata, Kata ya Ukata ambayo pia iko mbali na huduma na eneo ambalo pia lina mlipuko wa magonjwa mara kwa mara.

Mheshimiwa Spika, ajira; naomba kipaumbele kitolewe kwa wanaojitolea na wale waliohitimu mafunzo vyuoni miaka ya nyuma, maana ikiwa yupo mwombaji wa ajira amemaliza chuo mfano mwaka 2015 na mwingine mwaka 2020 basi yule wa mwaka wa nyuma kumaliza apewe kipaumbele ikiwa na kigezo cha umri wa mwombaji tukitambua ajira Serikalini unataka umri usiozidi miaka 45.

Mheshimiwa Spika, maombi ya watumishi; Halmashauri ya Wilaya Mbinga ina upungufu mkubwa wa watumishi katika sekta ya afya na elimu. Upungufu ni mkubwa zaidi katika afya kiasi cha zahanati kubaki na mhudumu mmoja tu. Mfano kuna upungufu wa zaidi 80%; waliopo ni 20% Idara ya Afya, hivyo ombi langu katika ajira hizi mpya tupewe kipaumbele kuongezewa watumishi katika sekta ya afya na elimu.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa TARURA; naomba waongezewe fedha hususani TARURA Halmashauri ya Mbinga DC kutokana na ukubwa wa eneo, lakini hali ya milima na mabonde kiasi cha kuhitaji madaraja na mifereji mingi. Niombe waongezewe fedha kwa kutekeleza miradi ya barabara zitakazoweza kupitika msimu mzima wa mwaka tofauti na ilivyo sasa barabara nyingi zinapitika kiangazi na kufunga kupitika wakati wa masika kutokana na kukosa madaraja na tope kuwa jingi.