Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya ufinyu wa muda naomba kuwasilisha kwa maandishi maeneo ambayo nilitaka kuyasema jana lakini muda wangu ukaisha kabla ya kusema.

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kuhusu ujenzi wa barabara ya Akheri kutoka Sangis hadi Ndoombo; ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya kuanzia Sangis kwenda Akheri hadi Ndoombo ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete aliyoitoa mwaka 2012 wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mbunge wetu Marehemu Jeremiah Solomon Sumari. Ujenzi wa barabara hii umeanza lakini kazi inaenda kwa kusuasua sana licha ya kwamba kipande kilichopatiwa fedha mwaka huu wa fedha 2022/2023 ni kilometa 1.2 tu. Maoni yangu ni kwamba urefu wa kipande kilichopatiwa fedha ni kidogo mno ukizingatia kwamba ahadi hii imechukua muda mrefu zaidi ya miaka kumi kutekelezwa. Nashauri Serikali iongeze fedha kwa TARURA barabara hii imalizike ndani ya uhai wa Bunge hili la Kumi na Mbili.

Pili ni kuhusu ujenzi wa vivuko; mwaka 2020 wakati wa Bunge la Bajeti Serikali iliahidi kutoa fedha kutoka kwenye Mfuko wa Maafa ili kujenga upya madaraja na vivuko vilivyosombwa au kuharibika kipindi cha mvua nyingi za mwaka 2019/2020. Kata nyingi kule Arumeru Mashariki mipaka yake ni mito na vivuko vingi vilisombwa. Naomba pia Serikali itekeleze ahadi yake kwa kuipatia TARURA fungu maalum kutoka kwenye Mfuko wa Maafa ili vivuko vilivyosombwa vijengwe upya.

Tatu; utekelezaji wa ahadi za viongozi; ahadi za viongozi wakuu: -

(a) Barabara ya Akheri kutoka Sangisi hadi Ndoombo iliyotolewa mwaka 2012 (kazi inaendelea);

(b) Ujenzi wa barabara kilometa tano kwa kiwango cha lami Usa River iliyotolewa mwaka 2015 (utekelezaji bado); na

(c) Ujenzi wa barabara ya Kingori kwa kiwango cha lami kilometa 33 ilitolewa mwaka 2020 (utekelezaji bado).

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.