Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, hivi karibuni Serikali ilitoa mwongozo kuwa shule za Serikali na binafsi zisitishe bweni kwa madarasa ya tano, nne hadi chekechea lakini hadi sasa kuna shule zimeendelea kulazimisha watoto wa madarasa haya kukaa bweni. Jambo hili linaleta mashaka na wasiwasi kuhusu usalama wa watoto wetu hususan suala la maadili ambapo hivi sasa kuna ukatili mkubwa dhidi ya watoto wadogo hususan mashuleni. Natolea mfano wa Shule ya Msingi na Elimu ya Awali ya Ndameze iliyopo mkoani Kigoma. Ni vyema Serikali ifuatilie utekelezaji wa agizo ililotoa ili kulinda usalama wa watoto wetu.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni upungufu wa watumishi hususan walimu na idara ya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Jimbo la Singida Kaskazini, upande wa walimu tuna upungufu wa walimu 900 na zaidi na upande wa afya tuna upungufu wa watumishi 316. Ni ombi kubwa kuwa katika ajira zilizotangazwa, Halmashauri ya Wilaya ya Singida nayo ipatiwe watumishi hawa, na upande wa utawala pia tunao upungufu mkubwa wa watendaji wa kata na vijiji.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine naomba fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa boma la Kituo cha Afya Ngimu ambalo limekaa miaka 14 sasa. Pia ukamilishaji wa jengo la OPD la Kituo cha Afya Kinyagigi ambapo wananchi wameshapaua, kilichobaki ni umaliziaji tu ambao makadirio ni shilingi milioni 100 tu. Aidha katika Hospitali ya Wilaya tunaomba kupatiwa standby generator ambalo litasaidia wakati umeme umekatika. Mara kadhaa umeme unapokuwa umekatika wagonjwa wamekuwa wakipata tabu hususan wanapojifungua na wale wanaohitaji kupumua kwa mashine.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.