Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nampongeza Rais kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika majimbo yetu. Nampongeza Waziri na Naibu Mawaziri wake kwa kazi nzuri wanazofanya. Mchango wangu utajielekeza katika maeneo manne; kwanza ni utekelezaji wa mradi wa TACTIC uongezwe kasi katika makundi yote matatu ya mradi; na pili, Serikali ije na sheria ya ugatuaji (decentralization) ili kuwa na mipaka ya kisheria kuhusu majukumu ya Serikali za Mitaa na Serikali Kuu.

Tatu, Halmshauri ya Mji wa Nanyamba ina upungufu mkubwa wa watumishi, mahitaji ni watumishi 744 na waliopo ni 133 sawa na asilimia 19. Naomba kuwe na mpango wa haraka kupunguza upungufu huo; na nne, walimu wanaojitolea wapewe kipaumbele wakati wa kuajiri walimu wapya.