Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. MWANTUM M. ZODO: Mheshimiwa Spika, naendelea kuishauri TAMISEMI kuwapatia watendaji wa kata mafunzo ya muda mfupi kupitia Chuo cha Utumishi wa Umma. Watendaji wa kata na vijiji ndio wasimamizi wakuu wa shughuli za Serikali kwenye maeneo yetu, watendaji wa kata na vijiji ndio wasimamizi wakubwa wa kila siku wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo yetu, watendaji hawa ndio wakusanyaji wakuu wa ukusanyaji mapato ya halmashauri zetu, watendaji wa kata na vijiji ndio wasimamizi wakuu wa uchaguzi kwa ngazi za kata na vijiji. Mkurugenzi, Mkuu wa Idara wala DC hawawezi kuwa site kila siku, badala yake wanatekeleza majukumu yao ya kiofisi ya kila siku. Watendaji hawa ndio Serikali ya kwanza mwananchi wa kawaida anayokutana nayo kila siku, lakini pia ndio wanaoishi na wananchi.

Mheshimiwa Spika, tuendelee kukuomba Mheshimiwa Waziri kutafuta fungu kwa ajili ya mafunzo haya ya watendaji kama Kamati ilivyopendekeza.