Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja hii ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora. Ukiangalia majukumu ya Msingi ya Wizara hii ni kutengeneza Miundo, Sera na Nyaraka ambazo ni rafiki zinazotoa hamasa kwa watumishi wetu. Hata hivyo, kuna Miundo ya Utumishi ya muda mrefu, Muundo wa toka mwaka 2002 na miundo mingine. Hii miundo imebaki kuwanyanyasa watumishi au kuwa threat kwa watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu watumishi wa umma kila mmoja anaajiriwa kwa muundo wake. Kwa mfano, watumishi wanaoajiriwa kwenye wa Muundo Mwandamizi, nitoe mfano kama Maafisa Kilimo, anaajiriwa kama Agriculture Field Officer au Afisa Kilimo Mwandamizi ana mahali pake akifikia bar, kwa mfano TGS G hawezi kuendelea ndio mwisho wa muundo wake. Mtumishi huyo akienda kujiendeleza akasoma, pengine ametoka diploma ameenda degree, badala ya kupata promotion sasa kama alikuwa TGS G atoke pale aende H muundo unamrudisha mpaka pale kwenye TGS D. Sasa TGS D mpaka kwenda TGS E anahitaji miaka mitatu, kama kweli muundo utampandisha smoothly. Akitoka D kwenda E miaka mitatu, akitoka D kwenda hiyo G yake miaka mitatu mingine. Sasa mpaka kwenda kumvusha mpaka kwenye H ni miaka tisa mpaka 12. Hivi Muundo huu ni rafiki kwa wafanyakazi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa unam-frustrate mfanyakazi ambaye tayari alishajiendeleza mwenyewe na anajiendeleza kwa ajili ya kutoa huduma bora. Iko hivyo hivyo hata kwa watumishi wa Afya. Ma-nurse wetu wanaosoma RNDA au train nurse darasa la saba amehamasishwa ameenda kusoma form four amemaliza, ameenda kuchukua diploma, wanapopata diploma akirudi kwenye utumishi, muundo ule una-frustrate wanashindwa kwenda mbele na wenzao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu cha kushangaza, sijui kwa nini tunatenga watumishi? Muundo huu ukienda kwa Walimu, Mwalimu mwenye diploma akienda kusoma degree, yeye anahama moja kwa moja na ule muundo wa watu wenye degree, hakuna kinachomrudisha nyuma kama maeneo mengine. Sasa ifike muda basi niiombe Wizara hebu wa- review hii miundo. Miundo ambayo sio rafiki kwa watumishi, miundo inayokandamiza watumishi na kuwa-frustrate. Kama sasa hivi sio hitaji, umefika muda sasa ku-review na kuachana nayo na kuangalia namna nyingine ya ku-motivate mtu ambaye ameamua kujiendeleza, ukitegemea sasa hivi dunia inaenda na teknolojia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, lakini inakuwa mbaya zaidi kama mtumishi wa Idara tofauti ameenda kusomea kitu tofauti, hapo ndipo unammaliza kabisa. Kwa mfano, Mwalimu, yeye toka mwanzo wito wake ulikuwa unamtuma labda kusomea kitu kingine Afisa Utumishi au Mwanasheria, akajiendeleza yeye mwenyewe, maana huko nyuma atakuwa alisaidiwa na wazazi, pengine fursa ilikuwa ni kwenda Chuo cha Elimu na fursa ya kupata utumishi ilikuwa ni hiyo, lakini atakapokuwa mkubwa na mshahara wake amejiendeleza na pengine halmashauri imempa nafasi ya kuwa labda Mwanasheria, anarudishwa kwenye muundo ule wa kuanza wa degree, lakini hata ile personal salary yake inafutwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshawahi kuona mtumishi anapunguziwa mshahara, anaenda kuanza kwenye mshahara wa chini. Hii miundo mingine naomba sasa ufike muda tu-review, tuone ni namna gani ambapo watumishi sasa wawe na furaha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni hili muundo wa hivi karibuni wa Halmashauri sijui restructuring maana nilishawahi kuuliza huko nyuma kama swali. Pengine nia ni njema halmashauri kwa ajili ya kubana matumizi imebadilisha muundo, ilikuwa na idara 13 na vitengo, sasa hivi imebana zile idara zimebaki idara tisa. Kwa maana hiyo kuna Idara zimeunganishwa kama za Kilimo na Vitengo vingine kama vya Uchaguzi vimefutwa, Idara kama ya Fedha imekuwa kitengo, can you imagine idara ya fedha ndio mkono wa Mkurugenzi pale. Sasa pengine sio shida, sijui kama kuna utafiti wa kutosha uliofanywa kuunganisha Idara za Kilimo na Mifugo pamoja na zingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa stress zinatoka kwamba mtumishi ambaye alishawahi kuwa Mkuu wa Idara sasa unampoeleka chini ya Mkuu wa Idara nyingine, it is enough torture to him (psychological torture) yaani hawezi kuwa happy kufanya kazi chini ya idara nyingine. Vile vile na ufanisi utakuwa chini, kwa sababu taaluma ya kilimo ni tofauti na taaluma ya mifugo. Haiwezekani mtu wa mifugo ukimpa asimamie kilimo kwa vyovyote vile atakuwa bias. Niombe wafanye review. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwangu tatizo ni kwamba, kama tulikuwa tunabana matumizi, hawa Wakuu wa Idara na Vitengo ambao vitengo vyao vimefutwa kwa mfano Afisa Uchaguzi, huwezi kumnyang’anya mshahara wake na stahiki zake za Mkuu wa Idara, ataendelea kubaki nayo. Kwa hiyo, ataendelea kupata mshahara wa Mkuu wa Idara na zile stahili ambapo hakuzifanyia kazi na huwezi kumwacha pale kwa sababu atakuwa hayuko happy. Sasa sijui wamejipangaje kumjengea job satisfaction huyu mtu aweze kuwa happy sasa kuendelea? Kama alikuwa ni Mwalimu, utamrudisha kwenye chaki, alishakuwa Mkuu wa Idara, fikiria ukimrudisha kwenye chaki, ni kweli ataenda kufanya utumishi vizuri? Napendekeza, pengine ikibidi kwa hawa watumishi ambao idara zao zimefutwa labda wapelekwe kwa RS.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile, nataka kusema kuhusu watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wanavyopatikana. Watumishi hawa RS (Sekretarieti ya Mkoa) kazi yao kubwa ni kusimamia watumishi pamoja na Wakuu wa Idara katika halmashauri. Hata hivyo, hebu ona unamwajiri mtu kijana aliyetoka chuo unamweka pale kwenye Sekretarieti ya Mkoa. Anatoka huko anaenda kusimamia miradi ya halmashauri. Kama ni Engineer wa Umwagiliaji anakuja yule technician wa umwagiliaji aliyeko kule kwenye halmashauri ana knowledge kumshinda yeye. Ndio maana wakija wakubwa, akija Waziri Mkuu au Waziri mwingine kukagua miradi anakuja kukuta miradi mingine iko chini ya kiwango na lazima ina mapungufu. Sasa jiulize kama RS (Sekretarieti ya Mkoa) ilikuwepo pale walitoa ushauri gani huko?

Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza wa-review utaratibu wa kupata Sekretarieti ya Mkoa kwa sababu wao ni wasimamizi wa miradi yote ya halmashauri pamoja na Wakuu wa Idara, wafanyiwe kama wanavyofanyiwa Wakuu wa Idara, wawe na experience ya kufanya kazi kwa miaka sita kama Wakuu wa Idara na wafanyiwe vetting, halafu wapate promotion ya kwenda Mkoani. Hii itawa-motivate pia watumishi wetu wengine kwenye halmashauri wajue kwamba watumishi wakifanya vizuri kuna promotion ya kwenda Mkoani. Hiyo itasaidia sana, naomba hilo waliangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza na kusema ukweli nampongeza na Mama, kipindi hiki ndipo tumepata nafasi za ajira kuliko kipindi kingine chochote. Nashukuru kwamba ajira nyingi zimekwenda kwa Walimu pamoja na watumishi wa afya, lakini kuna Wizara tunazisahau…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Yustina Rahhi kwa mchango wako, unaweza kuunga mkono hoja kama ulidhamiria. (Kicheko)

MHE: YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)