Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi na mimi niongee mawili, matatu kwenye suala zima linahusu watumishi. Tutakubaliana kwamba maendeleo yoyote, iwe ya nchi, iwe ya taasisi, iwe ya familia inategemea nguvu kazi, pale ambapo unakuwa na nguvukazi ambayo si tu hairidhishi lakini pia inakuwa imekatishwa tamaa na kulegalega, hata kwenye familia binafsi huwezi ukapata mafanikio. Tuangalie mfano mdogo wa private companies ni kwa jinsi gani zinaweza zikafanikiwa vis a vis The Government activities au government other things, unajua ni kwa nini? Kwa sababu wanaweza kuwa motivated.

Mheshimiwa Spika, nitaanza kutoa mfano mdogo tu Mheshimiwa Waziri ametuambia kwamba kuna watumishi ambao wanakuwa ni zaidi ya mwaka mmoja wanadai mishahara, tunategemea mtu afanyeje kazi anadai mshahara kwa mwaka mmoja, totally impossible! Mchukue mtu huyo huyo mpeleke kwenye private company au private business anaweza kufanya kazi bila kulipwa? Kwa nini tunapaswa ku-assume kwamba watu wanaweza kufanya kazi za umma wanaweza kufanya kazi Serikalini bila kulipwa na wakaendelea kufanya kazi? Tunaendelea kujidanganya.

Mheshimiwa Spika, nataka niseme Mheshimiwa Waziri na nitataka baadae nitatoa Shilingi atuambie ni kwa namna gani hili suala halitajirudia la Watumishi wa Umma kudai malimbikizo, kudai mishahara wakati huo huo tunategemea walete productivity, hicho kitu hakiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kabla sijaenda mbali nitataka niseme kwa kifupi kuna suala zima la TASAF. Kila mmoja anelewa umuhimu wa TASAF, na swali langu ninalotaka ku- pause ni kwa kiwango gani TASAF inaweza kuwa endelevu kama inategemea kuwa financed na donors au misaada kwa maana Wizara haitengi fedha kwa ajili ya TASAF? hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili ni kwa nini TASAF imekuwa inatumika kama siasa kwenye maeneo yetu, huwa napokea simu nyingi sana wananiambia Mheshimiwa Mbunge nimetishiwa kuondolewa TASAF kwa sababu nimeonyesha nina interest ya Chama fulani. Mimi nadhani haya masuala yafikie mwisho, siyo mara ya kwanza linasemwa hapa Bungeni na siyo mara ya pili na siyo mara ya tatu unless Waziri atuambie kwamba TASAF inatumika kama kiboko kwa ajili ya interest za siasa za Chama Fulani. Nadhani ifikie mwisho na niseme bayana kama itatokea Watendaji wanataka kuwa-punish watu kwa sababu ya interest fulani za vyama na nini kwa kuwanyima TASAF hatutakubali, na tutakaa kuipinga sasa kwa sababu itakuwa haina tija au itabidi itengenezewe jina jingine kwamba hii siyo TASAF bali ni motivation ya kujiunga na itikadi fulani hilo naomba niliweke wazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuje kwenye suala zima la upungufu wa watumishi….

SPIKA: Mheshimiwa Anatriopia nieleweshe vizuri kuhusu jambo hili, kwa sababu niliwaona Wabunge hapa ambao ni wa Chama cha Mapinduzi na walisimama kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri maswali kuhusu TASAF kwamba kuna watu ambao hawamo na wanastahili. (Makofi)

Hii hoja ya kwamba ambao hawamo wanaokutafuta wewe lazima wahusishe hoja ya kutokuwemo na Chama fulani inatokana na nini labda au kwa sababu wewe ni wa Chama kingine kwa hivyo wakikupigia lazima kuna uhusiano na Chama chako. Kwa sababu nimeona nimeyasikiliza maswali hapa na Mheshimiwa Naibu Waziri amejibu maswali mengi sana kuhusu TASAF na hao ni Wabunge wa Chama cha Mapinduzi, hebu nieleweshe mimi ili nijue jambo hili limekaa vipi, Mheshimiwa nakuomba uendelee.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, katika maeneo ambayo tunatoka ukionekana una-element za Upinzani moja kati ya kitu ambacho wanaambiwa tutakutoa TASAF na the next month hapokei fedha, anachopaswa kukifanya ni kwenda kufuatilia mchakato ni wangapi wana uwezo wa kwenda kufuatilia mchakato kama akikubali imeishia hapo, lakini kama ni mtu fighter anasimama firm anapambana mpaka anarudishwa kwenye TASAF.

Mheshimiwa Spika, point ninayotaka ku-make…

SPIKA: Mheshimiwa Waziri nimekuona nitakupa nafasi. Unajua Mheshimiwa Anatropia mimi nisingependa Bunge hili lifikie mahali kwa sababu siku moja niliwahi kusema hapa hatuelekei kufanya maamuzi lakini sasa tunaelekea kufanya maamuzi ukituweka kwa sura hiyo, nimeuliza hivi Wabunge kuna Mbunge mmoja sema sikumbuki ni nani, aliyesema kwake kuna watu ambao wameondolewa kwenye TASAF wakati vigezo bado wanavyo ni nani? Ni Mbunge gani? nadhani Mheshimiwa Sekiboko pale na anatoka Tanga na yeye ni Mbunge wa Viti Maalum. Tanga hakuna Jimbo la Upinzani kule, sasa mimi nawaza kule wale wananchi wa Tanga aliowasemea anatoka Korogwe siyo? Hebu washa kisemeo. Ulisema ni Korogwe au ni wapi?

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, ni Korogwe Mkoa wa Tanga, Korogwe Mjini.

SPIKA: Sasa Korogwe Wabunge wote wawili wa Wilaya ya Korogwe ni wa Chama cha Mapinduzi na kule wapo ambao walikuwepo na sasa wameondolewa kwenye mfumo na ndiyo Wabunge walikuwa wanasema wameondolewa kimakosa kwa sababu vigezo bado wanavyo. Hii hoja ya kwamba wanaokupigia wewe wameonesha alama pengine ama namna fulani kwamba ni wa Chama.

Waheshimiwa Wabunge, nisingependa Bunge lifikie hapo mahali na sababu ni za msingi kabisa, Wabunge wa CCM kama wanaongea na wewe unazungumza hoja yako ni ya msingi, kwamba watu wanostahili wapewe na wasiostahili waondolewe na vigezo vitumike vile vilivyopo, sasa ukiiweka kisiasa kidogo inakuwa mtihani. Hapo ndiyo shida yangu ilipo.

Mheshimiwa Anatropia.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na mimi wito wangu ninaotaka kauli ya Mheshimiwa Waziri aseme bayana watu wasionewe au wasipewe kwa sababu iwayo yoyote na kigezo kibaki kilivyo leo. Haya maeneo tumetofautiana uelewa. Korogwe wanaweza kuwa waelewa na eneo jingine vipi maeneo ambayo wengine tunatoka? Ndiyo nataka kauli iwe firm kwamba mtu apewe TASAF kwa sifa ya yeye kuwa na uhitaji wa TASAF full stop, hiyo ndiyo call yangu.(Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mbunge, nadhani hujanielewa vizuri, Mbunge wa jimbo unalotoka wewe ni wa Chama gani? Jimbo unalotoka wewe walimchagua Mbunge wa Chama gani?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, Tume ilimtangaza Mbunge wa CCM.

SPIKA: Ndiye aliyechaguliwa. Kwa hiyo, hoja ya kwamba walioko kule wakikupigia wewe ni wa CHADEMA hilo ondoa kabisa, TASAF hata Majimbo ya CCM yameulizwa maswali hapa ndani. Kwa hiyo, iondoe kabisa hiyo sijaelewa ambapo wewe hunielewi ni wapi. Ukiiweka tu kisiasa kwamba kuna mtu hapewi kwa sababu ya siasa humu ndani Wabunge wa CCM wameuliza maswali, ukisema kuna mtu anaondolewa kwa sababu ya kisiasa pia unakuwa hauko sawasawa kwa sababu Wabunge wa CCM wameuliza vivyo hivyo.

Kwa hiyo, wewe changia kwamba kuna hiyo changamoto kwenye TASAF na sote tumeisikia hapa, usiiwekwe kisiasa kwa sababu TASAF kwa maelezo mimi nikikaa hapa mbele nimewasikia na leo uzuri swali lilikuwepo hakuna mtu aliyeuliza swali kwamba kuna mtu alionyesha kadi ya chama fulani ndiyo akapewa au chama fulani ndiyo akanyimwa Hapana! Kwa sababu hata wewe nikikuambia uthibitishe huna uwezo huo. Ama unao Mheshimiwa Theonest ndiyo maana nilikuwa nakuwekea mazingira hayo mchango wako uwe wa jumla kwa changamoto za TASAF na siyo kwamba wenye changamoto wana viashiria vya Chama fulani hapana.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru niendelee. Naomba mchango wangu uwe jumla katika changamoto…

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Ngoja kwanza Mheshimiwa Rose lazima uitwe kwanza ndiyo uanze kuzungumza. Mheshimiwa Anatropia kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Rose Busiga. (Kicheko)

TAARIFA

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa taarifa Dada yangu kwamba kwa uzoefu nilionao kuhusu TASAF. TASAF wanapochaguliwa ni Kijiji husika, kinakuwa na Mkutano wa hadhara, Mwenyekiti wa Kijiji pamoja na Mtendaji wa Kijiji wanapokuwa pale kwenye mkutano wanakijiji wenyewe wanajua maisha ya wenzao ndiyo wanachagua pale. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Anatropia Theonest unaipokea taarifa.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, naendelea. Kwa sababu wakati mwingine haya mambo huwa yanashamiri sana ikifika wakati wa maneno mengi, nakushukuru sana niendelee.

Mheshimiwa Spika, kuhusu changamoto ya watumishi. Kuna changamoto kubwa na CAG ameainisha dhahiri kwamba kuna upungufu wa asilimia za kutosha, anasema silimia 35 tukiongela kwenye kada nzima ya elimu.

Mheshimiwa Spika, kwa tathmini ambazo kwa projection za kuwa na wanafunzi 50 mwalimu mmoja katika shule ya msingi, lakini mwalimu mmoja wanafunzi 20 kwa shule ya sekondari tumeona bado ni changamoto na hatuoni dalili ya kuifikia kama kuajiri bado kunaendelea kwa kusuasua. Hii hapa imekuwa na impact kubwa, nitatoa mfano. Katika taarifa aliyoitoa kwa mujibu wa ripoti ya CAG inaonyesha wanafunzi asilimia 66 wamepata Division Four mpaka Division Zero na hiyo inatokana na kwamba wanafunzi wengi hawajaweza kupata access ya mwalimu. Walimu hawajaweza kufundisha vya kutosha kwa sababu madarasa yetu ni makubwa na hiki ni kilio nikitoe kwenye eneo langu ambalo ninatokea kwenye Mkoa wangu wa Kagera hususani Wilaya ya Kyerwa, kuna changamoto kubwa ya walimu.

Mheshimiwa Spika, niombe katika uajiri unaoenda kuufanya katika ajira zilizotangazwa tupewe kipaumbele, moja haya ni Majimbo ya Vijijini hii nitoe ni general call, Majimbo ya Vijijini na maeneo mengine lazima yawe na motisha ukilinganisha na maeneo ya Mjini. Kwanza kila mtu anajaribu ku-avoid vijijini, iwapo mishahara ya walimu na watumishi wanaofanya kazi vijijini ikiwa juu pamoja na allowance za posho za kufundisha posho za maeneo inaweza kuvutia kwa wingi haya maeneo kuwa na walimu wa kutosha kinyume na hivyo.

Mheshimiwa Spika, pia tuna changamoto ya walimu wa kike ni maeneo mengi nchini. Walimu wa kike ni muhimu kwa sababu mkumbuke kwamba katika level ya chini wanafunzi wengi pia ni wa kike, wanahitaji assistance ya walimu wa kike lakini wanahitaji role models ya walimu wa kike. Tunawezaje kuwa-motivate walimu wa kike kubaki kwenye maeneo yetu. Moja ni lazima tuwaongezee posho, mbili ni lazima tuwape mazingira ambayo wanaona kwamba ni rafiki, nyumba za watumishi na maeneo.

Mheshimiwa Spika, nataka pia niongelee kukosa motivation kwa watumishi kama nimeeleza tangu awali nikianza na kuwa na malimbikizo makubwa ya mishahara, siyo hiyo tu hata wanaosataafu unatumikia leo una uhakika kwamba hata ukija kustaafu utalipwa posho zako na kiinua mgongo, hiyo michango yenyewe ambayo mamlaka na taasisi mbalimbali zimekuwa haziwasilishi zimekuwa ziki- accrue interest from time-to-time.

Mheshimiwa Spika, nataka nitoe mfano mmoja tu, kwa ajili ya kutopeleka hayo makato Halmashauri kadha wa kadha zimepata faini mfano mmoja Halmashauri ya Muheza ililipa twelve million, Biharamulo six million, Kaliua five million, Mlele five million, kwa ku-sum up zimetumika zaidi ya Billion 260 katika kulipia faini za kutokusanya michango. Sasa leo hatuajiri kwa sababu hatuna fedha lakini hizohizo fedha zinaenda kutumika kwa ajili ya interest za kutopeleka fedha za makato mbalimbali kwenye taasisi husika, na hilo ni swali la jumla ambalo naweza kulitoa hapa, tujiulize sisi kama Serikali mjiulize ninyi kama Wizara mnataka ku-achieve nini? Kusimamia watu kupeleka hayo makato ili msilipe interest na badala yake hiyo pesa ndogo tuitumie kuajiri watumishi? Au tubaki nazo mezani ili kesho tulipe interest? Kupanga ni kuchagua! (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Anatropia kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu.

TAARIFA

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Spika, nataka tu nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika mambo makubwa na mazuri yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita ni kuongeza motivation kwa watumishi na hasa kupitia haki na stahiki zao.

Mheshimiwa Spika, ninazo taarifa rasmi na ni za uhakika mwaka 2020/2021 Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati anaingia madarakani alikuta bajeti ya Watumishi kupandishwa madaraja ilikuwa ni watumishi 91,000 lakini mpaka Januari mwaka huu, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amepandisha madaraja zaidi ya Watumishi 263,555. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wakati Dkt. Samia Suluhu Hassan anaingia madarakani alikuta tatizo kubwa la malimbikizo ya mishahara, mpaka mwezi Januari Tarehe 30, alikuwa amekwisha kulipa malimbikizo ya mishahara kwa watumishi zaidi ya 116,000 katika Serikali hii. Kwa hiyo, ninachotaka kumpa taarifa Mheshimiwa Mbunge ni kwamba siyo kweli Serikali haioni umuhimu wa haki na stahiki za watumishi ili kuwapa motivation katika kufanya kazi zao za kila siku. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Anatropia unapokea taarifa hiyo?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kitu ambacho napaswa nikiweke wazi mtumishi kupandishwa daraja siyo hisani, ni kwa mujibu wa Kanuni na Utaratibu lakini pia ni increment kwa kazi aliyoifanya. Huwezi kuajiriwa leo ukalipwa sawa sawa na yule aliyekaa miaka Mitano, huo ni wajibu wa Serikali kupandisha madaraja ndiyo tunayaongea hapa.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Anatropia kuna taarifa nyingine kutoka kwa Mheshimiwa Halima Mdee.

TAARIFA

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, nilikuwa nampa taarifa Mheshimiwa Anatropia kwamba madai ya Watumishi wa Umma mwaka 2019/2020 ilikuwa Bilioni 334, mwaka 2020/2021 yakaongezeka yakafika Bilioni 429, taarifa ya juzi ya CAG inaonesha madeni ya Watumishi yamefika Bilioni 509, ni taarifa tu nilikuwa nampa Mheshimiwa.

SPIKA: Mheshimiwa Anatropia unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, naipokea sana, na hilo ndiyo ninalolisema leo. Tunaweza ku- achieve tunachokitaka kama tuna right people on the ground. Ni lazima watumishi wawe motivated kwa kulipwa malimbikizo, kwa kupandishwa madaraja, kwa kulipwa fedha za uhamisho, kwa kulipwa posho kadha wa kadha ambazo zipo kwa mujibu wa utaratibu. Hivyo ndivyo watakavyofanya kazi. Tunakwama wapi? Nilikuwa naangalia clip moja inayoonesha ni namna gani nchi kama Singapore iliweza kufika ilipo. Jibu lilikuwa moja, lazima uwe na watumishi sahihi, ndiyo utaweza ku-achieve hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)