Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa hotuba ya Waziri, ukurasa wa 28 Serikali imelipa madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi 14,398 yenye jumla ya shilingi 25,655,898,954.61 hadi Machi, 2023. Vilevile madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi wa umma 2,942 waliokoma utumishi wao yamelipwa, na kwamba kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Februari, 2021 hadi Machi, 2023 Serikali imelipa madai ya malimbikizo ya mishahara 119,098 yenye thamani ya shilingi 204,420,741,285.25.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri alieleze Bunge hili tukufu madai hayo inayosemekana yamelipwa yanatokana na kiasi gani kinachodaiwa na cha muda gani? Na kiasi gani bado hakijalipwa na kina muda gani? Hii inatokana ukweli kwamba bado madai ya watumishi ambayo hayajalipwa ni mengi na malalamiko yamekuwa mengi sana.

Mheshimiwa Spika, moja ya jukumu ambalo Wakala wa Ndege za Serikali iliongezewa mwaka 2016 ni jukumu la kuratibu ununuzi wa ndege na kukodisha kwa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), halikadhalika kusimamia mikataba ya ukodishwaji wa ndege hizo kwa niaba ya Serikali. Ningependa kufahamu kwa mwaka wa fedha 2023/2024 tunatarajia kutumia kiasi gani kwa ununuzi wa ndege? Lakini pia kumekuwepo na malalamiko toka ATCL, moja ya sababu linalolifanya shirika husika kujiendesha kwa hasara ni mkataba mbovu wa ukodishaji na matengehezo ya ndege. Nini kauli ya Serikali kuhusiana na hili na hatua gani inatarajia kulichukua kunusuru shirika letu la ndege?

Mheshimiwa Spika, naomba nipate ufafanuzi wa kina kwenye maeneo hayo mawili.