Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na mimi kunipa nafasi hii kuweza kuchangia Ofisi hii ya Muungano.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru Mwenyezi Mungu na mimi kunijalia kupata nafasi hii. Nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anazozifanya katika nchi yetu. Nichukue nafasi hii kumpongeza Dkt. Hussein Ali Mwinyi Rais wa Zanzibar kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuisimamaia nchi yetu lakini pia kwa kuusimamia Muungano wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwashukuru watangulizi wa Muungano huu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pamoja na Marehemu Aman Abeid Karume, kwa kweli walikaa wakafikiri suala kubwa sana kuungana na kutufanya sisi kuwa ndugu. Wao waliunganisha udongo au walichanganya mchanga, lakini Muungano wetu kwa sasa sisi tumechanganya damu. Kwa kweli sisi sasa hivi ni ndugu hatuwezi kutengana na hatuwezi kugombana; mambo mengine madogo madogo yatakayotokea hayo ni mambo ya kibinadamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tumpongeze mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuusimamia Muungano huu. Kuna watangulizi wake walipita, yeye ni Rais wa Sita lakini amefanya mambo makubwa sana, na shahidi ni Mheshimiwa Waziri ambaye amezungumza kuwa kero nyingi za Muungano zimetatuliwa. Hilo tulijua litafanyika kwa sababu Muungano huu sasa hivi umetufanya sisi kuwa ndugu, hatutakiwi tugombane, tuzozane wala tuoneane, lazima tuwe pamoja, na mama yetu hilo ndilo analolitaka. Mimi bado nitashikilia, kung’ang’ania kushikilia na kusema kuwa Mama Samia ni mcha Mungu, Mama Samia ni mkweli, bado nitaendelea kuzungumza suala hilo Mama Samia ni mkweli na ni mcha Mungu.

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu watangulizi walitangulia walizungumza kuhusu kero za Muungano. Mimi nasema kero zipo na zitaendelea kuwepo madhali sisi ni binadamu; lakini nasema kwa kipindi cha Mama Samia mambo mengi yatatatulika; yametatuliwa lakini ataendelea kuyatatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu walizungumza kuhusu kero ya Bandarini. Bandarini pana matatizo makubwa sana; kuna wanawake wanaotoka Zanzibar wakati wa hizi Sikukuu wanakuja kununua vitu vyao vidogo vidogo Dar es Salaam, na tunasema nchi yetu ni moja, ni Tanzania, wakifika pale bandarini wanaadhibiwa sana na suala hili tulishalizungumza sana. Sisi ni ndugu, Mheshimiwa Waziri tunamwomba afike bandarini kama wale watu wa bandarini hawana elimu wakapewe elimu. Sisi tunazungumza ni ndugu lazima tukubaliane, kuna mambo mengine hayana haja ya kujitokeza sisi kuja kulizungumza humu. Ni sisi wenyewe tujue hiki hakikubaliki, hili halikubaliki, lakini kumekuwa na unyanyasaji mkubwa bandarini wenzangu wamezungumza.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo mtu anakuja na TV yake moja, TV moja kweli ni ya kufanya biashara anakwenda kuzungumza na Watoto wake sasa hivi azam Alhamdulillah makero mengi mengi ma-stress yanaondoka kwa Azam tu, anakuja mtu TV ile ailipie kodi, tena anaambiwa ondoka, nimeshuhudia anaondoka. Ukienda kusema jamani mwachieni hayo matusi utakayoyapata.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tutakuwa tunavuruga Muungano na tunamvurugia mama yetu. Yeye ana nia nzuri kuutetea Muungano huu na bado anautetea na anaulinda kwa maslahi ya nchi yetu. Kwa hiyo na sisi tuliopewa nafasi lazima tuzisimamie kwa kuzitetea nafasi zetu na kuwatetea wananchi wetu. Wanawake wengi wanaofanya biashara ndogo ndogo wanadhalilika, wanateseka bandarini, biashara zao zinapotea, inauma sana. Hawa ndio wapiga kura wetu; na mwanamke tunasema sasa hivi ndiye mtetezi wa nchi hii, lazima tupewe kipaumbele. Muungano wetu ndio kama ni kioo chetu, kwa hiyo lazima muungano huu tuulinde, tuutetee, na msimamizi sasa hivi ni Mama, hakutuacha nyuma. Sisi tunasema hatuna malalamiko makubwa ya kuzungumza kuhusu Muungano huu maana yake tunasema sasa tumechanganya damu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika,asilimia kubwa ya Wabunge wa Zanzibar wanaokuja miaka mitano lazima anaacha watoto huku. Huku wanaacha Watoto, ndiko kuchanganya damu huku. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika,Kwa kweli Mheshimiwa mambo ya hizi kero, mambo madogo madogo yaondoke. Sisi kila siku tunazungumza tunapiga kelele tunazungumzia hayo kwa hayo yale kwa yale, hayapendezi. Muungano wetu nchi nyingi wanatuonea choyo au wanatuonea husuda, kwa kweli ni jambo la kusikitisha.

MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa, taarifa.

TAARIFA

MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kumpa taarifa dada yangu anaye changia hapa sasa hivi. Si kwamba wanaacha watoto tu, mimi mwenyewe hapa ni mtu wa Morogoro Mama yangu ni Mtu wa Zanzibar. (Makofi)

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Naibu Spika, umeyasikia maneno. Muungano huu hatukuchanganya udongo peke yake. Udongo bado utabakia kwenye kumbukumbu lakini sasa hivi tunasema Muungano huu tumechanganya damu. Tukizungumza hapa tukijifafanua asilimia kubwa tunasema sisi ni ndugu wa baba mmoja. Kuna mambo lazima tuyazungumze kiudugu, lazima tukubaliane isiwe kila siku tunapiga kelele Muungano Muungano. Muungano huu hakuna yeyote wa kuweza kuutengua kwa kusema huu haufai kwa sababu ukisema haufai mimi nikirudi Zanzibar huku na acha dada yangu, naacha bibi yangu, naacha shangazi yangu. Siwezi kwenda kule lazima huku nitarudi. Sisi sasa hivi tunakwenda free Zanzibar na Bara kwa sababu sisi ni ndugu.

Mheshimiwa Naibu Spika, utazunguka bara yote lazima utamkuta Mzanzibar yupo kazaa amejukuu kwa hiyo naunga mkono hoja. (Makofi)