Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza sana kwa kuja na Mwongozo na kanuni za biashara ya carbon. Hamasa ya kupanda miti ni kubwa, napongeza sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo na ufinyu wa bajeti yapo masuala ambayo kwa kushirikiana na sekta binafsi na asasi za kiraia tunaweza kufanikisha mengi. Na hapa nina ushauri ufutao: -

Kwanza, tukumbuke kwamba tumechelewa sana kama Taifa kunufaika na mifuko ambayo ninahitaja mara kadhaa, kama GCF, GEF, AP na kadhalika; na hii tukiwa honest inatokana na ukweli kwamba ndani ya Serikali tuna tabia na hulka ya kujifungia, yapo mambo lazima tufanye engagement, tuwe na partnership, ikiwa Mheshimiwa Rais ameonesha njia katika kushirikiana na sekta binafsi na asasi za kiraia na sisi tunao wajibu wa kufuata nyayo hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano katika COP 27 baadhi ya asasi na NGOs zilifanya jitihada za kukutana na Mfuko wa GCF, na tayari kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Climate Action Network wanayo concept note ya USD 380M jointly with ambayo fedha ikipatikana utekelezaji wa mradi utafanywa kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Wizara ya Maji, Mifugo na Mamlaka ya Hali ya Hewa. Mradi huu utatekelezwa katika mikoa 22 na mradi utawafikia karibu 70% ya wakulima wadogo, wafugaji na jamii za wavuvi na fedha hii zaidi ya 65% itakwenda Serikalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa taarifa nilizonazo GCF walithibitisha kupokea andiko wakashauri ili kukidhi vigezo, linapaswa andiko liwe kwenye luggage za kitaaluma kadri ya mwongozo vya GCF. Moja ya ushauri ni Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira wafanye mawasiliano na GCF kuomba support ya kupata Mshauri Mwelekezi na GCF wako tayari kulipia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu kwamba suala hili lipo kwenu toka mwaka jana mwishoni na uzuri linafanywa kwa ushirikiano na Wizara ya Afya, hata hivyo hakuna kinachoendelea. Huu ndio msingi wa hoja yangu kwamba tunachelewa sana kufanya maamuzi, tupunguze kujifungia, ninawasilisha kwa maandishi kwa sababu kwa maadili nisingependa kuyazungumza kwa kuongea, lakini nitashukuru ikiwa ushauri huu Serikali itaufanyia kazi kwa kuwa wepesi katika kushirikiana na sekta binafsi na kuwa wepesi kimawasiliano, tupunguze urasimu.

Pili ni kuhusu biashara ya carbon; napongeza sana kuja kwa kanuni na mwongozo, hata hivyo bado tunahitaji kuwekeza katika utaaalam na ushawishi. Suala hili linahitaji utaalam wa hali ya juu sana hasa katika kupiga mahesabu husika.Ninaamini kuwa tukijipanga vema, tunaweza tukapunguza kukata miti, kwa sababu wananchi ikiwa watanufaika na biashara ya carbon, watapanda miti zaidi na iliyopo, wataitunza kwa umakini mkubwa sana. Kwa hiyo, narudia tena ushirikishwaji wa sekta binafsi na NGOs ni jambo muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, zuio la matumizi ya mkaa 2024 vs uwekezaji kwenye nishati mbadala; Mafinga tulikuwa na viwanda vitatu vya kuzalisha mkaa (Briquettes charcoal) ambao ni bora na rafiki kimazingira. Hata hivyo katika viwanda hivyo, viwili vimefungwa, kimebaki cha Briquettes Energy Solution ambacho hata hivyo kinauza mkaa nje mpaka Ujerumani na uhitaji ni mkubwa sana. Ushauri wangu, viwanda vya aina hii tuwe na mpango mkakati wa kuvijengea mazingira rafiki ya kiuwekezaji, lakini kwa kuwa pia zinashiriki kukabiliana na uharibifu wa mazingira kwa sababu zinatumia mabaki ya mazao ya misitu, zinastahili kupata fedha kutoka mifuko husika, lakini pia kuna mkanganyiko kwamba fedha za carbon ni kwa ajili ya misitu ya asili, je, ukweli ni upi?

Mheshimiwa Naibu Spika, utaalam vs ushawishi wa kisiasa hasa kikanda; ili kupata fedha hizi kunahitajika utaalam lakini ushawishi wa kisiasa, hasa kikanda, kwa mfano kupitia EAC, SADC na hata AU, kwa sababu kutengwa fedha ni jambo moja, lakini kuzipata ni jambo la kipekee. Mfano mzuri ni Mradi wa Mabadiliko ya Tabianchi kule Simiyu, nyote mnafahamu mzunguko uliotumika kuzipata fedha hizo, nashauri ushirikiano ndani ya Serikali na nje ya Serikali na ndio maana nasisitiza lazima ndani ya Serikali tuwe open, tuwe sharp, tukubali ushauri na tuwe wepesi kufanya engagement, hii itasaidia sana kupata fedha kutoka mifuko niliyoitaja lakini pia tukijipanga na suala zima la Loss and Dama Fund kwa sababu majanga ni makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.