Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa fadhili zake kuu na neema zake za kila namna. Mwenyezi Mungu ambaye ametujaalia pumzi hata tukapta fursa ya kujadili Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyopeleka fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii pia kumpongeza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mheshimiwa Dkt. Selemani Jafo kwa namna anavyoingoza Wizara hii akisaidiana na Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii kupongeza Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), kwa kuja na mpango wa kujenga kuta katika maeneo yetu ya mwambao na katika visiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe mpango huu uwe endelevu na uangalie maeneo mbalimbali ya pwani ya nchi yetu. Niiombe Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) ifikirie kujenga ukuta ili kuzuia athari za kimazingira katika Mji Mkongwe wa Kilwa Kivinje ambao ulijengwa tangu wakati wa utawala wa kikoloni na sasa umebomoka. Kwa kufanya hivi tutaweza kuhifadhi ardhi ya mji huu na kufanya makazi ya watu, taasisi za Serikali na zisizo za Serikali, maeneo ya biashara na viwanda vilivyopo katika Mji wa Kilwa Kivinje, kuwa salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.